Wafilipi 2:10-11
  • KUKOMBOLEWA KUTOKA KWENYE NGUVU ZA GIZA na Emmanuel ENI SEHEMU YA TATU (PART 3)

    *Page 20*
    20
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu* jengo moja kubwa na refu lililofanana na jengo
    la mikutano. Tulipokanyaga
    ndani ya sakafuni tu sauti kutoka
    ndani ikasema: "*Muingizeni ndani"
    *Waliniingiza ndani kisha wakatoweka, na
    kuniacha peke yangu. Nilichokiona ndani ya ukumbi huu ni vigumu
    kueleza, lakini nitajaribu
    kuelezea kadiri nitakavyoweza. Ukumbi
    ulipambwa vizuri sana na ulikuwa mkubwa
    sana na mrefu kiasi kwamba ilikuwa
    ni vigumu kuona mwisho wake. Nilitembea mpaka katikati na ndipo niliweza wa
    kuona mwisho wake. Mwishoni
    kulikuwa na madhabahu. Kisha
    nikaona kiti cha enzi na na aliyekuwa ameketi
    juu ni mwanaume mzuri sana
    mwenye nguo inayong`aa kama jua. Akasema: *"Njoo!" *Lakini kwa sababu ya
    mwangaza wake sikuweza kwenda. Kila
    nilipojaribu kunyanyua mguu
    wangu nilianguka.
    Nilisimama, nikajaribu tena na nikaanguka.
    Ghafla mtu huyo akatoka kwenye kiti cha enzi alipokuwa
    amekaa,akahamia kwa juu kidogo nilipokuwa
    nimesimama. Kisha mikono miwili
    ikatoka nje ya mtu huyo,
    ikanishika kichwa changu na kunitikisa na mwili
    wangu wa kibinadamu ukajivua kama unavua nguo.. Na yule
    mimi mwenyewe sasa akasimama. Mikono
    akaikunja kama mtu anaye kunja nguo na
    akaitupa kwenye kona. Mtu
    yule akarudi tena kwenye kiti chake cha enzi
    na akakaa na kusema tena: *" Njoo! "*
    *Kutakaswa Kiroho*
    Nikatembea mpaka pale naye akasogea
    kutoka katika kiti cha enzi, akanyofoa
    miguu yangu mmoja baada ya
    mwingine na akamwaga kile kilichokuwa ndani yake, na akaiweka tena vizuri.
    akafanya hivyo pia kwenye
    mikono na akaiweka tena, Yaani ni hivi
    sehemu zote ambazo Malkia wa Pwani
    aliweka nguvu zake humo.
    Nikatafakari sana kwenye fikra zangu, huyu atakuwa nani na amejuaje kuwa
    maeneo haya ndiyo yalikuwa
    yametunza nguvu zangu. Baada ya haya
    alirudi tena kwenye kiti chake na
    akaniambia niende. Nilipoanza tu
    kutembea, vitu fulani vikaanza kuanguka kutoka kwenye mwili wangu , magamba
    yakaanguka kutoka katika
    macho yangu, nk, lakini kabla sijafikia
    madhabahu tayari vikaacha.
    Aliniuliza. *" UNAKWENDA WAPI ?"*
    Nikajibu, nikasema, "Ninaenda Onitsha kumuona rafiki."Akasema: *"Ndiyo,
    lakini mimi nitakuonyesha nini*
    *ulichopanga kwenye akili yako*. " Hadi wakati
    huu sikujua alikuwa ni nani,
    lakini jambo moja nililokuwa na
    uhakika nalo ni kwamba alikuwa mwenye nguvu zaidi kuliko nguvu zote
    nilizowahi kukutana nazo. Alisema kwa
    ishara na mtu ambaye aliamriwa kunionyesha
    mimi nini nilichokuwa
    nimedhamiria moyoni kukifanya. Mtu huyu
    alinipeleka kwenye chumba na akufungua kitu kama ubao. Kwa kweli, kama
    kulikuwa na njia ya kutoroka
    ningeweza kutoroka, kwani mbele yangu
    yaliandikwa yote niliyopanga kufanya
    dhidi ya Wakristo na mpango
    wangu dhidi ya kania la Assemblies of God, Silver Valley. Mtu huyu
    akanileta tena madhabahuni na akaniacha.
    Akatoka katika kiti cha enzi na akanishika kwa
    mikono yake na akasema kuwa
    anakwenda kunionyesha mimi
    mambo fulani. Tulipokuwa njiani Akasema: *"Mimi sitaki wewe upotee lakini
    nikuokoe na hii ni nafasi yako *
    *ya mwisho. Kama hautatubu na kuja
    kunitumikia, utakufa. *Nitakuonyesha
    makazi ya waliookolewa na
    waasi." Alivyosema hivyo, nikajua alikuwa ni *Yesu Kristo.*
    *Ufunuo wa Kimbingu*
    Tukaingia katika chumba fulani na akafungua
    kitu kama pazia. Niliona dunia
    nzima, watu na shughuli zote za
    kinachoendelea. Nikaona Wakristo na wasio wakristo wote wanafanya jambo
    moja au jingine. Tulikwenda
    kwenye chumba cha pili . Akafungua pazia
    tena na nilichokiona ilikuwa ni
    kitu mbaya kuonekana. Watu
    wamefungwa minyororo ! Aliwaita watu hawa " *wanafiki. *"Watu hawa
    walionekana ni watu wenye huzuni
    kubwa, Akasema: ". *Watabakia hivi mpaka
    siku ya hukumu "*
    Tulienda katika chumba cha tatu. Akafungua
    pazia na nikaona watu wengi wanafuraha na wakiwa wamevaa
    mavazi meupe. Wakati huu nikamuuliza : " Ni
    kina nani hao " Akasema: *"Hawa
    ni wale waliokombolewa *
    *wanasubiri ujira wao. " *Tulikwenda katika
    chumba cha nne na nilichokiona kilikuwa cha kutisha mno.
    ------------------------------
    *Page 21*
    21
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu* Ndugu msomaji, ni vigumu kuelezea.
    Ilionekana kana kwamba mji mzima unawaka
    katika moto. Kuzimu ni halisi
    na niyakutisha. Kama ulikuwa umefanywa
    kuamini kwamba Mbinguni na Kuzimu ni
    hapa duniani na kwamba hakuna maisha mengine mara baada ya kifo
    bali ni kuoza na kupotea kabisa,
    ni bora ukashauriwa vizuri hapa na
    sasa kwamba kuzimu halisi ni halisi na kuna ni
    kweli mbingu ipo!
    Usistaajabu Yesu Kristo alipokuwa hapa duniani Aliwaonya watu kuhusu kuzimu.
    Nasema tena , kuzimu ni halisi.
    Niliiona na ni mahali pa kutisha.
    Nikamwuliza : " Ni nini ?" Jibu lake lilikuwa :
    *"Hii imetayarishwa kwa
    ajili ya shetani na malaika wake na* *kwa walioasi" *Akataja kwa majina yao kama
    ilivyoandikwa katika Ufunuo
    21:8: "Bali waoga na wasioamini na
    haramu, na wauaji, na wazinzi na wachawi,
    waabudu sanamu na waongo wote,
    sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti ambayo ni mauti ya pili
    " .
    Tulipoenda katika chumba tano na Alipofungua
    pazia, nilichoona kinaweza tu
    kuelezewa kama UTUKUFU.
    Ilikuwa ni kama tunangalia kutokea kwa juu. Niliona *mji mpya*. Mji ulikuwa
    ni mkubwa na mzuri! Mitaa ni ya
    dhahabu. Majengo hayawezi kulinganishwa na
    kitu chochote katika dunia hii.
    Alisema: " *hili ni tumaini la watu*
    *wa Mungu. *Je, utakuwepo mahali pale "Haraka nikajibu" Ndiyo " Baada ya
    hayo tulirudi katika kiti cha enzi na
    Akasema: "!*Nenda kashuhudie nini
    nilichokufanyia "*
    Tena, alinichukua mpaka katika chumba
    kingine na alipofungua pazia nikaona mambo yote ambayo nilikuwa
    naenda kukutana nayo kwenye safari yangu
    ya kwenda Onitsha na Lagos na
    jinsi gani hatimaye atanikomboa.
    Baada ya hayo Akaniambia : *"Usiogope,
    nenda, nami nitakuwa pamoja nawe." *Aliniongoza,
    nje ya ukumbi
    na akatoweka kabisa, na mara nikaamka
    kwenye kitanda katika nyumba ya
    mwanaume mwingine. Nikapiga
    kelele, mtu na mke wake wakakimbia kutoka katika chumba chao. Wakachungulia
    na kisha wakaingia "Kwa nini
    niko hapa? " Niliuliza. Mwanaume yule ndio
    alielezea jinsi nilivyoanguka
    katika teksi na jinsi walivyonipeleka
    kwenye kanisa la Katoliki pale Owerri. Jinsi walivyomleta Daktari, ambaye
    alikuja na baada ya kunichunguza
    afya yangu alisema mapigo yangu yalikuwa ya
    kawaida na kwamba wanapaswa
    kusubiri na kuona nini
    kitatokea. Daktari akawapa uhakika kwamba nitapata nguvu tena. Ndipo
    alinichukua kwenye gari lake mpaka
    nyumbani kwake na alikuwa akisubiri. Pia alikiri
    kwamba hakujua kwa nini
    alimuamini Daktari na kwa nini
    alichukua jukumu la kunichukua mpaka nyumbani kwake.
    Waliniuliza jina langu na anwani ambayo
    niliwapa na baada ya hapo niliamua
    kukaa kimya na sikuwaambia
    uzoefu wangu huo. Nilikaaa kwa utulivu na
    familia hii yenye wema kwa siku mbili na kisha mtu huyu na mkewe
    walinipeleka mpaka kituo cha magari cha
    Owerri, ambapo nilichukua teksi na
    kwenda Onitsha. Yote yale Bwana
    alinionyesha kuhusu safari yangu yalitokea
    moja baada ya jingine. Nilichukua teksi nyingine ya kwenda Lagos.
    Jambo la kwanza asubuhi iliyofuata. Nilitii na
    kuondoka Lagos kuelekea Port
    Harcourt. Huwa najiuliza mara
    nyingi, kwa nini Bwana aliamua kuniokoa mtu
    kama mimi. Mtu muovu na muharibifu, wakala wa Shetani !
    Nilipata jibu katika maneno haya matatu:
    *Mungu ni upendo*. Hakika, Mungu
    ni Upendo! (1 Yohana 4:8 , 4:16)
    ------------------------------
    *Page 22* 22
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    *Sura6: Vishawishi na Ushindi*
    *« Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi
    nawajua, nao hunifuata. Mimi nawapa uzima wa milele; nao*
    *hawatapotea milele, wala hakuna mtu
    atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.»
    Yohana10: 27-28*
    Baada ya kubadilika na kwenda kwa Kristo,
    jambo la kwanza lililotokea ni kwamba zawadi zote kutoka baharini,
    darubini, TV, mashati, picha nilizopiga nikiwa
    ndani ya maabara za baharini
    na picha ya Malkia wa Pwani ambazo
    zilionekana katika gorofa yangu zilitoweka.
    Niliporudi Port Harcourt, nilikuwa na hamu ya kushuhudia kile Bwana
    alichonifanyia kwa ajili yangu lakini
    sikuruhusiwa ndani ya kanisa . Mke wa
    marehemu mjomba wangu, ambaye pia ni
    Mkristo, alinichukua mpaka
    kwa mchungaji mmoja, lakini swali alilouliza lilikuwa ni: "Je,ameleta
    karatasi?" Ilikuwa ni baadaye sana
    nilielewa kwamba karatasi ilikuwa ni 'barua ya
    uanachama. Barua ya
    uanachama inahusika vipi na ushuhuda
    wangu wa nguvu ya Kristo na kile amefanya kwa ajili yangu- Mungu,
    amenikomboa kutoka katika nguvu za giza
    na kuniingiza katika ufalme wa Mwana wake
    mpendwa, ambaye nimepata ukombozi
    kupitia damu yake, yaani,
    na hata msamaha wa dhambi zangu ? Nilihuzunika, baada ya kujua kwamba Shetani
    haruhusu waumini wachanga
    kwenda na kushuhudia, hasa wale
    ambao hapo awali walikuwa washiriki wakubwa
    katika shughuli zake , na
    anafanya kila kitu kuzuia shuhuda hizo. Tena nikakumbuka, ni dhahiri Bwana aliniagiza
    "*kwenda na kushuhudia kile
    amenifanyia *" na hapa nilikutana
    na kipingamizi. Labda ilikuwa bado si wakati
    wake. Hivyo niliamua kuachana
    na kutoa ushuhuda wangu kwa mtu yeyote. Nilisafiri na wafanyabiashara
    watatu kutoka Aba kwenda Togo kwa
    safari ya kibiashara. Pale
    nilinunua bidhaa yenye thamani ya N160,000
    (Mia moja na sitini elfu za
    Naira). Kati ya pesa hizi pesa yangu binafsi ilikuwa ni shs N70,000 na nyingine yote
    iliyobakia N90 ,000
    nilikopa kwa wafanyabiashara wa Aba.
    Miongoni mwa mambo niliyonunua ilikuwa ni
    furushi la kamba, madawa
    mbalimbali ( hasa antibiotics ) , sindano, vipimajoto, nk
    Nilipofika mpakani mwa Nigeria, Tulishikiliwa
    kwa ajili ya ushuru wa
    Forodha na baadaye tulitakiwa kutoa
    rushwa. Tulikataa na bidhaa zilikamatwa ikiwa
    ni pamoja na zile za wenzangu. Miezi michache baadaye, Ile
    mizigo ya wenzangu ilitolewa, ila yangu
    haikuruhusiwa. nilirudi baadaye na
    nikaambiwa kulipa N40,000, lakini
    nilipoangalia mali yangu ile niligundua kwamba
    bidhaa zote muhimu, kama furushi la kamba, sindano, madawa,
    nk, tayari vilikuwa vimeibiwa. Nilitathmini bidhaa
    iliyobaki na nikajua
    kwamba kulipa N40,000 kwa ushuru
    itakuwa tu ni kuongeza hasara, hivyo niliamua
    kuachilia bidhaa iliyobaki. Wafanyabiashara ambao niliwakopa fedha
    walianza kunifukuzia. Baadhi
    waliwaita polisi, wengine walichukua
    sheria mkononi mwao na wakapanga
    kunifanyia kitu kwa maisha yangu.
    Suluhisho pekee lilikuwa ni kufunga akaunti yangu Bank na kutumia fedha zote
    nilizokuwa nazo kulipa madeni
    yote. Kwa neema ya Mungu, nililipa
    yote isipokuwa N1,000 ambayo ilikuwa ni kwa
    ajili ya mwenye nyumba wangu
    Lagos. Nilikuwa mufilisi kabisa na nilikopa hata 20k kwa ajili ya nauli ya teksi.
    Nilikwenda kwa wakristo wachache niliowajua,
    ili kutafuta msaada wa
    kuniwezesha kuanza upya. Hakuna
    aliyesema ndiyo au hapana, badala yake
    walinisihi niende siku inayofuata kila mara nikachoka kwa habari ya
    kutafuta msaada. Sikujua neno la Mungu
    pamoja na kuchanganyikiwa katika
    moyo wangu nilisoma Biblia bila
    kuelewa. Wakati bado natafakari nini cha
    kufanya, nilipokea simu ya haraka kutoka kijijini mwangu. Nilikimbia
    nyumbani na kukuta kwamba jengo dogo
    nililokuwa nimeanza kujenga lilikuwa
    limevunjwa na mjomba wangu
    ambaye pia alikuwa ametishia kuniua. Asili
    yangu ya kale ndani yangu ilishtuliwa. Nikakumbuka wakati nikiwa
    na jamii ile ya baharini (secret society), jinsi
    alivyokuwa akiniogopa na
    alikuja kwa magoti mbele yangu. Lakini
    sasa alijua nimebadilika (jinsi alivyojua sikujua
    kwani sikuwa nimesafiri kwenda nyumbani tangu nilipobadilika)
    ------------------------------
    *Page 23*
    23
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu* na sasa alinitishia. Nilimuita Bwana na
    nikasema: "Basi, wewe umeniokoa
    mimi na kuniacha nimevurugika na
    kuruhusu adui zangu kufurahia juu yangu! "
    Nililia kwa sauti nikadhamiria
    kurudi kwenye ile jamii ya kichawi. Angalau wanaweza kuniokoa kutoka katika
    kuchanganyikiwa kote huku na pia
    watafundisha mjomba wangu
    somo ambalo hatasahau maisha yake yote.
    Ingawa nilifanya uamuzi huu,
    nilikuwa na hofu mbili ndani yangu 1. Wakati nilipokuwa nabadilika, Bwana
    aliniweka wazi akaniambia: " *Hii ni
    nafasi yako ya *
    *mwisho. *" Ukirejea tena kwenye jamii ile ina
    maana ni kifo, sio tu kifo
    cha kimwili lakini pia cha kiroho.
    2. Kama nikibakia katika Bwana, mjomba
    wangu alikuwa anatishia kuniua.
    Nilichanganyikiwa na nilihitaji msaada. Nilikuwa
    mjinga wa neno la Mungu na
    kamwe sikujua kile ambacho Neno linasema kwa habari ya hayo juu. Ndugu
    msomaji , utagundua hapa kwamba
    nilikuwa na mchanganyo
    huu wote kwa sababu ya ukosefu wa
    mfuatiliaji nikiwa bado mchanga.
    Kuwafuatilia waongofu wachanga ni muhimu sana na Wakristo wanapaswa
    kuchukulia hili kwa umakini. Kama unajua
    huwezi kufuatilia muumini
    mchanga, tafadhali usiende kushuhudia. Yesu
    Kristo alisisitiza hili mara
    tatu Alipomuuliza Peter: " Simoni, mwana wa Yona, wanipenda mimi zaidi kuliko
    hawa? ... Lisha kondoo wangu.
    "Wengi wa waongofu wapya
    wanarudi nyuma kwa sababu ya kukosa
    ufuatiliaji mzuri. Kama unampenda Yesu,
    jali kondoo wake! *Vita na shetani*
    Katika kipindi hiki mawakala wa Malkia wa
    Pwani walianza kunitafuta sana.
    Niliteseka sana katika mikono yao.
    Nilikuwa na ndoto mbaya. 1 Mei 1985, mwezi
    mmoja baada ya kuokoka saa 02:00 usiku, wengine katika nyumba
    walikuwa wamelala. Niliamshwa na mawakala
    hawa. Wakaniamuru kutoka nje ya
    nyumba. Nilitii, nikatoka nje
    na walinifuata nyuma. Ilikuwa kama yote
    yanayotokea ni ndoto, lakini hii ilikuwa katika uhalisia. Tulitembea
    mpaka juu ya ardhi ya maziko kanisa la
    Mtakatifu Paulo Anglican , off Aba
    Road, Port Harcourt.
    Tulipofika pale walisema: "Ni lazima urudi.
    Kama ukikataa tutakuua au kukufanya fukara. "Baada ya maelekezo
    haya waliondoka. Nikapata ufahamu wangu na
    kujishangaa nimefika vipi pale
    makaburini. Nikarudi kitandani na
    kulala. Waliamua kuwa wananishambulia
    mchana. Mara kwa mara, wakati natembea kandokando ya barabara
    walijaribu kupambana na mimi. Wengine karibu
    yangu waliniona napambana na
    hewa au kuniona nakimbia kama
    mtu anayefukuzwa.
    Mimi peke yangu ndiye niliewaona. Basi, walifanya hivyo kwa mara nne na
    wakaacha. Kisha kiongozi wao ,
    Malkia wa Pwani, achukua jukumu. Siku ya
    kwanza alikuja katika gari ambalo
    aliliegesha kando ya nyumba yetu.
    Alikuwa amevaa vizuri na kama kawaida yeye ni mzuri sana. Watu
    walionizunguka walimchukulia kuwa ni
    mpenzi wangu. Mara akaingia ndani nilijua
    alikuwa ni nani. Alikuja saa
    12.00 mchana wakati eneo lote lilikuwa
    busy kidogo. Akakaa chini na miongoni mwa mambo mengine aliyoyasema ni:"
    Unaweza kwenda kanisani
    kwako, amini chochote unachotaka kuamini,
    *lakini kama tu hautanitangaza*,
    nami nitakupa chochote kile katika
    maisha haya " Sikuwa nimejua maandiko hivyo nilimsikiliza na kumuangalia
    anatembea tembea pale. Aliomba
    na alijaribu kunishawishi nirudi kwake.
    Sikusema ndiyo au hapana kwake.
    Alisimama, akaenda ndani ya gari
    yake na akaondoka. Kama mara mbili hivi mke wa mjomba wangu
    alimkaribisha nyumbani kwake bila
    kujua alikuwa ni nani nami
    kamwe sikuwahi kumwambia mke wa mjomba
    wangu alikuwa ni nani. Ziara yake ya
    mwisho alibadili namna yake ya kunisihi. Wakati huu alinipa onyo kali
    akisema kwamba amejaribu
    sana kunibembeleza nirudi kwake na
    kwamba nimekuwa mkaidi sana, na kwamba
    hii ilikuwa ni ziara yake ya mwisho.
    Kama bado nakataa kurudi, atakuja mwezi Agosti ama kuniua , au
    kunilemaza au kunifanya maskini. Kisha
    akaondoka.
    Nilikuwa na hofu, hivyo siku moja nilikwenda
    kanisani na kumuita ndugu
    mpendwa. Nilimwambia matatizo yangu na mtazamo wangu juu ya baadhi ya
    washirika wa kanisa , nk Huyu ndugu
    alinipa anuani ya ofisi ya umoja
    ------------------------------
    *Page 24*
    24 *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    wa maandiko (Scripture Unions ) na
    akaniambia: *" Pale watanipatia msaada*"
    Siku hiyo ilikuwa ni siku ya
    mwisho kumuona huyu " ndugu." Sijawahi kumuona popote Port Harcourt mpaka
    leo. Nilichukua anwani na siku
    iliyofuata, nilichukua teksi mpaka No 108
    Bonny Street, ambapo zilikuwa
    ofisi hizo ni na kukutana na mchapaji
    ambaye alinipa robo ya mpangilio wa shughuli za Umoja wa Maandiko (SU)
    Kundi la Rumuomasi Pilgrims,
    wakiwa ndio karibu na mimi. Akasema: " Njoo
    siku ya Jumapili! " Nilikuwa
    pale katika Fellowship Centre -
    Shule ya St Michael's State , Rumuomasi - saa 8:00 mchana, bila kujua
    kwamba ibada inaanza saa 9:00 mchana,
    lakini nilikutana na kikundi cha maombi, hivyo
    nikajiunga nao .
    Baada ya ibada siku hiyo nilijua kwamba
    mahali pale palikuwa sahihi kwangu.Mungu akanipa msichana ambaye
    alikuwa kama mama kwangu, yeye alijitoa
    kikamilifu katika kunielezea Neno
    la Mungu na kunishauri pia. Ndugu
    wakaonyesha utayari na kunijali. Niliona
    Upendo wa kweli. Roho Mtakatifu alianza kunipa ufahamu wa Neno la
    Mungu na imani yangu ilikua. Lakini Malkia wa
    Pwani hakujionyesha kwa
    sababu aliwekwa wazi. Zaburi 91,
    Ulinzi wa Mungu, ulitimia katika maisha yangu.
    *Isaya 54:17*: "*Silaha yoyote itakayofanywa juu yako *
    *haitafanikiwa, na ulimi wowote utakaoinuka
    juu yako katika hukumu wewe
    utauhukumu. Hilo ndilo fungu la urithi *
    *la watumishi wa Yehova, na uadilifu wao ni
    kutoka kwangu," asema Yehova.. *"Hii pia ilitimia.
    Septemba 1985, Nilipokea ujumbe kuwa jina
    langu limeonekana kama msambazaji
    wa Silver Brand Cement,
    Lagos na kwamba nilitakiwa kufika ofisini
    tarehe 27/9/85.Niliondoka Port Harcourt tarehe 26/9/85 na kufika
    Lagos usiku. Asubuhi iliyofuata 27/9/85,
    nilikwenda ofisini nikaambiwa na
    Meneja Utumishi kuwa sehemu
    yangu ilijazwa na mtu mwingine. Akanieleza
    nifike siku iliyofuata tarehe 28/9/85 kumuona Mkurugenzi
    Mtendaji. Nilipokuwa njiani kuelekea nyumbani
    kwangu, nikipita njiani, mtu
    akaja kutoka nyuma na kunikaba
    na akajaribu kubana pumzi yangu na mdomo
    wangu kwa pamoja. Nilijitahidi kuokoa maisha yangu, na ingawa
    watu walikuwa wanapita, hakuna aliyekuja
    kuniokoa, lakini Bwana aliingilia
    kati. Wakati mimi bado najitahidi
    kwa mikono nikasikia akilia kwa sauti na
    kunisukuma mbali akisema : "Ni nani huyo aliyeko nyuma yako? "
    Alirudia mara ya pili na kutoweka. Kutoka kwa
    sauti nilijua alikuwa ni
    mwanamke lakini kamwe sikumuona ni
    nani. Nilichanganyikiwa na kupigwa na
    bumbuwazi. Hapa tena mwenye nyumba wangu alikuwa na
    hasira sana na akasema: " Kwa nini
    umekimbia na fedha ya kodi
    yangu?" Nilimsihi na nikajaribu kumuelezea
    kwamba kwa sasa mimi si kazi na
    nitamlipa fedha zake zote kwa haraka mara nipatapo fedha.
    Kwa jinsi alivyoonyesha nilifikiri suala hili
    limeisha. Siku iliyofuata
    28/9/85, nilikwenda na kukutana na
    Mkurugenzi mtendaji ambaye aliomba
    msamaha kwa kumpa nafasi yangu mtu mwingine. Alipokuwa bado
    anaongea kijana mmoja akaingia na kuniuliza:
    " Je, wewe sie Emmanuel?
    "Nikasema ndiyo ni mimi: "Ndiyo ,
    mimi niko. " Akasema: "Ndiyo, hatimaye
    tumekupata sasa! Je, umemaliza kukimbia? Tumetembelea mara kwa
    mara Port Harcourt na kugundua kwamba
    daima huwa unatembea na mama yako wa
    kiroho. Amekuwa kikwazo
    sana kwetu na sasa kwa sababu umekuja
    Lagos tumekukamata! Hautarudi tena Port Harcourt. Mimi ndiye
    nimechukua nafasi yako " Nikampa
    changamoto na kumwambia : " Huwezi
    kunifanya kitu chochote "
    Mkurugenzi Mtendaji alishangazwa na kile
    kilichotokea katika ofisi yake ! Nikaomba radhi mwenyewe na
    nikarudi nyumbani.
    Dakika chache baadaye nikasikia mlango
    unabishwa na NINA akaingia.
    Akaniuliza kama nilikuwa narejea Port
    Harcourt. Nikajibu ndiyo. Aliniomba nirudi kwao akanieleza kuwa kazi
    nilizokuwa nimefundishwa zilikuwa
    hazipatikana mtu wa kuzirithi: KOTIPARI
    ( katika lugha ya Kiyoruba ).
    Nilikuwa nimepatiwa mafunzo :
    - Kuwa juu ya mawakala wa nguvu za mapepo.
    - Kuwa juu ya " chumba cha bahari cha
    maelekezo, " kufuatilia matukio
    katika dunia, kutuma na kupokea
    ishara, na kuhamasisha majeshi, nk
    - Kuwa karibu na Malkia wa Pwani. Hii inahusisha si tu sherehe, sadaka ,
    utekelezaji wa kazi maalum
    ------------------------------
    *Page 25*
    25
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu*
    alizonituma, lakini pia mambo mengine
    magumu kuelezea.
    - Kwa msaada wa nguvu za giza , kuanzisha
    jamii mpya za siri(jamii ya
    kichawi) ambazo zitaonekana hazina madhara ili kuwavutia vijana na zaidi waendaji
    tu wa kanisani .
    Alisema, kama ataongozana naye, kilichokuwa
    kinanisubiri ni mara mbili ya
    baraka za kwanza. Alikiri kwamba
    walihusika kwa mali yangu kukamatwa na kuibiwa, pia kwamba wao ndio
    waliomchochea mjomba wangu
    kuharibu jengo langu na kutishia maisha
    yangu. Kwamba kama nikikataa
    kumfuata, wangefanya zaidi na
    kuhakikisha kwamba sitafanikiwa. Kwamba walikuwa wameamua kupambana mama
    yangu wa kiroho: "Kama
    tutampata yeye, tumekupata wewe" alisema.
    Wakati huo, Nilianza kumhubiria.
    akasimama na kusema:
    "Wanakudanganya, " Akaondoka. Hii ilifanyika jioni ya tarehe 28/9/85 .
    Mara dakika tano zikapita nikasikia mwingine
    anabisha. Wakati huu walikuwa
    watu wanne. Wakanionyesha
    ishara nitoke nje na nikajiona mwenyewe
    naanza kuwafuata. Tulitembea hadi katika nguzo 2 na mmoja wao
    akaniuliza: "Je, unatujua sisi? " nikasema
    hapana. Aliendelea kusema: "
    Tumeajiriwa na mwenye nyumba wako
    tukuue." Wakati anaendelea kuzungumza
    mmoja wao akatoa bunduki na mmoja akatoa sime. Sikujua cha
    kufanya, nilijua kuwa wataniua, lakini Mungu
    katika Njia zake za ajabu
    akafanya ishara ambayo ilinishangaza
    mimi na wenyewe.
    Mtu aliyekuwa na bunduki akanifyatulia risasi lakini hakukuwa na sauti. Mtu
    mwenye kisu akakitumia nyuma ya
    mgongo wangu lakini hakikuingia ila tu kililia
    kama mtu anamchapa fimbo
    mtu. Walikuwa na hofu kama mimi.
    Roho wa Mungu alikuja juu yangu na nikaanza kuhubiri. Watatu wao
    wakakimbia, lakini mtu wa nne akaanguka
    na akaanza kulia na kuniomba nimuombee.
    Sikuweza hata kujua nini cha kuomba
    wakati huo lakini nilisema tu:
    " Bwana, tafadhali msamehe, Msamehe bwana. Amina! " Aliyalitoa maisha yake
    kwa Kristo, Nilimpeleka kwenye
    kanisa la Pentekoste na alielezea kile
    kilichotokea kwa Mchungaji.
    Nilimkabidhi kwa Mchungaji na nikaondoka.
    Nilipoingia tu ndani ya nyumba mwenye nyumba akaja anakimbia na akapiga
    magoti akinisihi: " Tafadhali
    nisamehe. Nilidhani uliamua kukimbia kwenda
    Port Harcourt kwa sababu ya
    fedha yangu (N1,000).
    "Nilimsamehe na hatimaye tulikubaliana kwamba fedha ilipwe kwa awamu .
    Usiku huo, mida ya saa 08:00 usiku Bwana
    aliniamsha. Sikuweza kujua kwa
    nini niliaamka nikaenda sebuleni na
    nilichokiona ilikuwa ni kobe mkubwa
    ananifuata. Mara nikakumbuka shule ya kujifunza Biblia tulipokuwa Port
    Harcourt, juu ya nguvu katika neno. Ndipo
    nikasema maneno haya: " Kobe ,
    tangu nilipozaliwa , nyumba ya kobe
    ni ama kichakani au baharini, lakini kwa kuja
    ndani ya nyumba wakati madirisha na milango ni imefungwa
    umefanya dhambi, na kwa sababu hii ni lazima
    ufe. "Mara baada ya kusema
    hivi akatoweka kabisa. Nilikwenda
    chumbani na kulala. Mara ya pili tena, niliamka
    na kusikia kelele sebuleni. Nilikwenda na tazama mbele yangu
    ilikuwa ni kitu cha kutisha. Nikarudia maneno
    yaleyale na mara baada ya
    kusema: "Kwa kutenda dhambi hii
    lazima kufa, " kikatoweka pia. *Wakati wa
    safari hii ya Lagos niliona wema, ukuu wa Mungu na uaminifu*
    *wake.*
    Asubuhi iliyofuata tarehe 29/9/85, nilichukua
    basi zuri sana mpaka Port
    Harcourt. Nilipofika Ore ,basi likagonga
    mti. Liliharibika kidogo lakini hakuna mtu aliyejeruhiwa. Dereva akalivuta
    kwenye barabara na akaendelea
    kuendesha, basi likaanza kuyumba kutoka
    upande mmoja wa barabara hadi
    mwingine. Nikakumbuka vitisho vya
    NINA, hivyo nikasimama katika basi, na kuhubiri nilihitimisha kwa kusema :
    "Ni kwa sababu yangu mimi haya
    yanayotokea. Lakini tangu sasa , hakutakuwa
    na ajali mpaka tufike Port
    Harcourt, katika jina la Yesu ! "Na mimi
    nikakaa. Kwa kweli, wakati nimeketi nilishangaa, kitu gani nimekisema. Na
    hivyo ndivyo ilivyokuwa. Gari
    lilitembea
    vizuri
    mpaka
    Port Harcourt.
    Hakukuwa
    na
    ajali
    zaidi
    au kuharibika.
    Biblia inasema sawa kuwa*;"Mtu yeyote
    akishambulia, haitakuwa kwa maagizo
    yangu.Yeyote atakayekushambul*
    *ia ataanguka kwa sababu yako."(Isaya 54:
    15). *Wao ( Malkia wa Pwani na mawakala wake ) walijaribu, lakini
    kwa sababu mkutano wao haukuwa katika
    Bwana bali kinyume na mtoto wake
    ,wote wakajikwaa na kuanguka.
    "Pindi adui atakapokuja kama mafuriko ya
    mto, Roho wa Mungu atainua kiwango dhidi yake" (Isaya 59: 19).
    Nampa Mungu utukufu wote kwa ajili ya
    kujionyesha mwenye nguvu kwa niaba
    yangu.
    ------------------------------
    *Page 26* 26
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    *Sura7: Shughuli za mawakala wa shetani*
    « *Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya
    damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu *
    *wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya
    katika ulimwengu wa roho. Kwa
    sababu hiyo twaeni silaha zote za *
    *Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya
    uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.»*
    *Waefeso. 6: 11-12*
    Kitabu hiki hakitakuwa kamili kama mbinu
    mbalimbali za uendeshaji wa
    mamlaka hizi hazitawekwa wazi. Pia
    ni muhimu kwamba aina mbalimbali ya namna na jinsi zinavyojitokeza ziwekwe
    wazi.
    Jambo moja li wazi nalo ni kwamba ni shetani
    atakuchochea uamini kwamba
    yeye ni hadithi tu za kufikirika au
    mawazo ya uovu ambayo ni rahisi, au atakufanya uone zaidi sana kwa habari
    ya nguvu zake na mamlaka ya
    Mungu iwepo chini. Biblia inasema: " *Kwa
    maana kushindana kwetu sisi si
    juu ya damu na nyama; bali ni juu*
    *ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo
    wabaya katika ulimwengu wa roho.*
    Biblia inasema kwamba silaha za Wakristo
    dhidi ya shetani na mawakala wake
    " *si za mwili, bali zina uwezo*
    *katika Mungu hata kuangusha ngome, tukiangusha mawazo na kila kitu
    kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya*
    *Mungu , na tukiteka nyara kila fikira ipate
    kumtii Kristo" *(*2 Wakorintho
    10: 4-5). *Tena maandiko yanasema:
    wazi *" Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa ili azivunje kazi za
    Ibilisi" (1 Yohana 3: 8). *Yesu baada
    ya kuzivua enzi na mamlaka, alifanya onyesho
    la waziwazi, alishinda dhidi
    yao .
    *"Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa
    chako," (Mithali 6:2)*.
    Hivyo mtoto wa Mungu ni lazima kuwa makini
    kukiri neno la Mungu, ambalo
    Mungu ameahidi ataharakisha
    kulifanya. Kuna ukiri mara tatu umesemwa katika neno la Mungu
    1. Ungamo la Uongozi wa Kristo.
    2. Ungamo la imani katika Neno, katika Kristo
    na katika Mungu Baba.
    3. Kukiri dhambi.
    Tunaposikia neno "kukiri ," sisi kwa urahisi tunafikiria kwa habari ya
    dhambi. Kamusi inafafanua kukiri ni :
    1. Kuanzisha kile kitu tunaamini.
    2. Kushuhudia kwa kitu ambacho tunakijua.
    3. Kushuhudia ukweli ambao tumeridhia .
    Kwa hiyo inapaswa kusikitikiwa kuwa tunapotumia neno kukiri (confession)
    kwenye fikra zetu tunafikiria
    dhambi. Mwandishi yuko hapa kukutia moyo
    mtoto wa Mungu kuanza leo kukiri
    kile Mungu amesema. hata
    wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na
    Kristo; yaani, tumeokolewa kwa
    neema na akatufanya tukae katika mbingu
    (juu sana zaidi ya enzi na mamlaka)
    katika Yesu kristo. Kwa hiyo
    Wakristo wanapaswa kutambua ambapo wamekaa. Wanapaswa kujua kwamba
    wanatembea katika urefu huo, juu
    ya Shetani na mawakala wake. Bwana Yesu
    Kristo amewapa ninyi nguvu zote na
    mamlaka ili kwa hizo tupate
    kuwa washirika wa uzima na utauwa (2 Petro 1 : 3).
    Mungu hakuwa na kusudi la kwamba
    mazingira yawatawale watoto wake, badala
    yake neno la Mungu katika
    kinywa cha Mkristo ni lazima kidhibiti hali/
    mazingira yake. Mungu alisema katikaYer. 23:29 akisema: "Je*, si*
    *neno langu kama moto? asema Bwana, na
    kama nyundo ivunjayo mawe vipande
    vipande?" *Wakristo,
    Namaanisha waliozaliwa mara ya pili,
    wanapaswa kutambua kuwa wakati jina la Yesu linatamkwa, kile
    kinachotoka nje ya vinywa vyao ni moto.
    Mkristo anaposimama juu ya mamlaka
    aliyopewa na Kristo na anatoa
    amri kwa jina la Yesu, moto hutoka katika
    kinywa chake na pepo lolote kudhibiti hali husika ni lazima kutii. Yesu
    yu hai leo ili kuangalia kwamba kila neno lake
    linakuja kupita. Tena,
    nataka kuonyesha ukweli muhimu kuwa
    ------------------------------
    *Page 27* 27
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    Wakristo wengi wanatazama kijuu juu , na hiki
    ndicho ambacho Shetani
    anatumia. Yesu, baada ya Peter kumsema kwake kwa habari ya ule mtini uliokauka baada
    ya kulaaniwa na Bwana ,
    alisema:
    (Matthew's account) *"Amin, nawaambia

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate