Wafilipi 2:10-11
  • JINSI KANISA LILIVYOTEKWA NA SHETANI

    Enyi mataifa yote nawaandikia waraka huu kama vile mimi Nabii Hebron nilivyofunuliwa na YESU WA NAZARETI mambo haya ambayo yanaupata  ulimwengu kwa kiasi kikubwa cha hatari hata pasipo wakristo kujielewa wapo katika MUNGU au shetani wakiwa wamefungwa fahamu zao hata wasijitambue na hata ule mwisho waje wakahukumiwe pamoja na lucifa japo wakristo hawapendi.
    Ninapowaeleza kuwa wakristo wanaenda kwa waganga wa kienyeji wakifikiri wanaenda katika nyumba za ibada kuombewa na watumishi wa MUNGU kwa idadi kubwa kumbe sivyo kabisa. Wanajikuta wanaenda kwa waganga wa kienyeji hao hao ambao wanajiita manabii, mitume, wachungaji, wainjilisti, waalimu na wengineo wenye huduma sita na kuendelea. Nitaelezea kwa ufupi na hakika utaenielewa na ukielewa hautaenda tena kwa waganga wa kienyeji bali utawafuata watumishi wa kweli wa MUNGU ili uonane na MUNGU.
    a.      Kila mtumishi anayejiita kwa cheo chake na yeye yupo katika mtandao wa freemason au illuminati halafu anaongoza kanisa na waumini na matawi yake, hawa ni wachawi na wewe mkristo unayoenda akuhudumie, akuombee pamoja na mengineyo, uelewe haujaenda kanisani bali umeenda kwa mganga wa kienyeji.

    b.     Watumishi wanaowatoa watu vitu kama mawe, nywele, chupa, na vinginevyo hao ni waganga wa kienyeji (ni watu ambao ni waganga wa kienyeji wakajiita ni watumishi ili wawateke watu na mali zao kwa kutumia kivuli cha jina la utumishi kumbe yeye ni mganga.

    c.      Watumishi wanaozini na waumini hao ni waganga wa kienyeji, siyo watumishi wenye roho ya MUNGU, ndani yao ipo roho ya uganga ya kipepo. Tazama hata watu wengi waliokwenda kwa waganga wa kienyeji wengi wao wanazinigi na mteja wake akiwaeleza miungu imesema waingiliane  kimwili na hata sasa mnayajua haya siyo mambo mageni.

    d.     Watumishi wanaonyang’anya watu mali zao, vitu vyao, wake, na kutoa huduma za kiroho kwa kuchaji watu pesa, kuwaeleza watu wasaini katika magari yao na nguo zao ndio watoe pesa wabarikiwe, hao ni waganga wa kienyeji 100%

    e.      Mafundisho tofauti na biblia ya Mwenyezi MUNGU inapokuwa tofauti uelewe unaenda kwa mganga wa kienyeji sababu wao ndio wapogo kinyume na MUNGU, na mtumishi anapokuwa kinyume na MUNGU na yeye asimcheke mganga wa kienyeji au kumchukia sababu hao ni moja na tena ni rahisi sana mganga wa kienyeji ambaye hajiiti mtumishi kuokoka na kwenda mbinguni kuliko anayejiita mtumishi lakini yupo kwa kivuli cha mganga wa kienyeji. (Utawajuaje? chunguza matendo yao).

    NOTE:
    Yapo mambo mengi ila haya yatakupa picha angalau uelewe umeendaga kwa mtumishi wa MUNGU au kwa mganga, picha umeipata. Na madhara yake ni watu wamechoka na ukristo wakaona YESU hayupo katika makanisa, ni sababu watumishi wengi zaidi tayari wapo katika upande wa shetani wanaganga na makanisa yao katika ulimwengu wa roho yanaonekana ni nyumba ya shetani. Sasa swali, je? YESU anafanya kazi na watumishi waganga wa kienyeji? Jibu, hapana. Ila mapepo ya michango, harambee ndio yamejaa makanisani kuwafilisi wanadamu, sasa mpone roho zenu.
    Sema BWANA YESU naomba unisamehe. Nilifikiri naendaga kwa mtumishi wako kumbe nilienda kwa mganga wa kienyeji pasipo kujua. Nanikaandikiwa jina langu katika vitabu vyao vya shetani badala ya mbinguni. Nisaidie YESU, uniokoe, nichomoe na vitu vyangu sasa hivi. Niongoze ulipo wewe. YESU WA NAZARETI WA KWELI. Amen.
    NABII HEBRON.

    Posted by Prophet Hebron



     

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate