Wafilipi 2:10-11
  • JE, UNAJUA KUZIMU NI WAPI?


    JE UNAJUA KUZIMU IPO KATIKA ARDHI YA NCHI ZIPI KATIKA RAMANI YA DUNIA?

    BWANA YESU ASIFIWE, YESU WA NAZARETI aliye ndiye mwana wa pekee wa MUNGU ambaye ndiye aliyenituma kuukomboa ulimwengu na mamlaka yake ya ajabu, leo mtapata jibu ambalo najua hamjui, katika haya mawili;

           I.            Hakuna anayejua mbinguni ilipo.

        II.            Hakuna anayejua kuzimu ipo wapi katika ulimwengu huu tunaoishi.

    Ila sasa nitaelezea tu kwa leo kuzimu ni wapi na ipo katika ardhi na nchi Fulani. Watu wengi wanafikiri kuzimu ipo chini kila mahali, hapana. Kuzimu ni kweli ipo chini na urefu wake ni kuanzia ardhi ya kwanza hadi ya milioni mianane (800,000,000 km) urefu wa kutoka duniani hadi mwisho. Ila katika hizi km serikali ya joka kuu hawakai mahali pamoja wanaishi mbali mbali, ila wanaishi karibu karibu, ni joka kuu yeye yupo katika ardhi ya 300,000,000 km, na lusifa yeye yupo katika ardhi ya 299,500,000, na roho mchafu ambaye aliitwa Maxwell yeye aliishi 299,000,000, ukiagalia utaona hawa wapo karibu karibu ila hao wengine wote wapo katika ardhi ya 100,000 laki moja.

    Haya yote alinifundisha mwalimu wangu na mwokozi wangu YESU WA NAZARETI ili niupindue ufalme wa shetani. Mimi kama Hebron sikutegemeaga  kwenda kuzimu au kuja kuwa mtumishi wa MUNGU ambaye hata MUNGU alimjua siku zote mpiganaji lazima uwe na maelekezo ya vita, na mimi nilipewa na kamanda mkuu ambaye ndiye YESU WA NAZARETI pamoja na malaika wa vita (Mikaeli). Nakuja kuelezea kuzimu ilipo sababu hata mimi nilifikiria kuzimu ipo chini ya miguu yangu au ya ardhi yeyote, kumbe siyo. Ila niliyajua haya pale ambapo aliponituma YESU kwenda kuzimu kuharibu ufalme wa shetani na joka kuu, hayo niliyoyafanya kuzimu nitaelezea siku nyingine, ila endelea kusoma makala ya Nabii Hebron, utafunguka zaidi. Shetani alishauteka ulimwengu 98% na mpaka sasa mataifa yote mfunguke, injili 98% katika ulimwengu wote ilikuwa inaongozwa na roho mchafu, mpinga kristo, au injili ya uongo, nah ii ilitokana na watumishi kumgeuka MUNGU badala ya kujenga ufalme wa MUNGU sasa hivi wanaubomoa ufalme wa MUNGU, na kanisa kukosa mwelekeo na YESU wa kweli, akabakia yesu wa uongo.

    Katika ramani ya ulimwengu huu na kabla ya kwenda kuzimu YESU alinionyesha ilipo na njia zao na wanapitia wapi na katika kimwili ni wapi, japo watu hawajui. Kuzimu ipo kama ilivyo huku duniani, ipo bahari, visiwa, mabara na miji na yapo makanisa ya shetani (joka kuu) ila nimeyabomoa yote na kuyachoma moto sababu hawa manabii wa uongo ndipo walipokuwa wanapata hizo nguvu za kuwadanganya wanadamu huku, na mtaona kila aliyetumia uchawi ataporomoka myaonapo hayo muelewe ndio wale ambao Nabii Hebron anatuelezea. Katika ardhi hii kuzimu ipo chini ya bara la Asia, ipo chini ya mji wa Lagos, ipo Sudan, ipo katika mji wa London, na Russian Federation, Australia, Madagascar, Somalia, America (katika jimbo moja), Syria, Libya na Egypt. Na vipo visiwa ambavyo sijavitaja. Kwa wale freemason, wachawi, manabii wa uongo, wao haya siyo mageni sababu ndizo njia za kwenda kwa mungu wao. Ila ipo habari njema, malango haya nimeshayafunga yote, na sasa watu watamjua MUNGU wa kweli na watamjua mungu wa uongo na injili ya kweli.

    Nawaeleza YESU anarudi, maneno haya ninayowaeleza mataifa yote siyo ya Hebron, ni kauli katika kinywa cha YESU WA NAZARETI, mrejeeni yeye, okokeni na muishi maisha matakatifu. Miaka 1000 imeshaanza tayari sasa wakati wowote ni unyakuo, atawanyakua wale waliookoka peke yake na kuishi maisha matakatifu. Msidanganyike na mafundisho ya uongo eti unajiita mkristo lakini hautaki kuokoka, nawaeleza habari njema, ili uwe mkristo ni lazima uokoke, kinyume na kuokoka wewe ni mkristo jina tu sababu kiunganishi yaw ewe kuwa mkristo ni uokoke. Watu wengine wanaona wameokoka ila mtumishi aliyemuongoza sala ya toba kumbe anaongozwa na yesu wa uongo. Na kama ni hivyo na wewe pia siyo mkristo, leo sema BWANA YESU WA NAZARETI naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniokoe na kuniandika jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele, simtaki yesu wa uongo na yesu wa unyang’anyi, michango, sanamu, ubatizo wa watoto wadogo, nakutaka wewe, karibu ndani yangu, uniongoze wewe kuanzia sasa. Amen.

    NOTE:

    Utashangaa sana ukiona baadhi ya watumishi wengi cheki passport zao hizo sehemu wameenda, hao wanaotumia nguvu za giza. Sasa wanapoenda katika nchi hizo huwa wanaenda kwenye njia za kwenda kwa joka kuu kuzimu, wanapewa mapepo na miujiza ya kiepo, wanakuja kuwanajisi wanadamu wasiende mbinguni. 98% ya watumishi wa kanisa wanaoenda katika hizo nci huenda kuingia kuzimu wala siyo kingine. Nimeyafunga hayo malango huo ndio mwisho wao, YESU WA NAZARETI NI MFALME, NI JEMEDARI anawapenda ndio sababu amenifunulia hayo mpate kuelewa ili muwe huru.

    Zaidi karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE. Nawapenda mataifa yote karibuni nyie mumrejee YESU wa kweli na akae ndani yenu na mumpokee awe BABA yenu na muwe salama.

    Nabii hebron.

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate