Wafilipi 2:10-11
  • KUKOMBOLEWA KUTOKA KWENYE NGUVU ZA GIZA na Emmanuel ENI SEHEMU YA PILI (PART 2)

    *Page 10*
    10
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema aliojaliwa na Mungu*
    Akanipeleka mpaka kwenye kiwanda kikubwa
    na ghala kubwa na kisha akanileta
    kwenye nyumba yake binafsi.
    Pale alikaa kuniambia: "Mimi ni Malkia wa
    pwani (queen of the coast) na ningependa sana kufanya kazi na wewe.
    Nina kuhahidi nitakupa utajiri na vyote
    vinavyokwenda pamoja nayo, ulinzi
    na vyote vinavyokwenda na hayo,
    uzima na 'malaika' atakayekuongoza wewe. "
    Akabonyeza kidude na mwili wa binadamu mbichi ukaja (katika vipande) ndani
    ya trei(sahani) na tukala pamoja.
    Akaamuru boa (nyoka) aje na akaniambia
    nimmeze.sikuweza. Alisisitiza lakini
    sikuweza, ninawezaje kumeza
    nyoka aliyehai tena aina ya boa. Akutumia nguvu yake na nikammeza. Haya
    yalikuwa ni maagano matatu: *mwili*
    *wa binadamu na damu*, *boa(nyoka) *na
    *malaika mapepo *walikuwa pale siku
    zote ili kuhakikisha hakuna siri
    iliyowekwa wazi. Lakini 'pepo' alipewa uwezo wa kuniadhibu
    kama nikienda tofauti na pia
    kiniletea chakula kutoka baharini
    wakati wowote nikiwa hapa duniani. Niliahidi
    kumtii siku zote daima. Na
    baada ya ahadi hii alinipeleka na sehemu nyingine ya bahari, Hii sasa ilikuwa ni
    kisiwa. Kulikuwa na miti na
    kila mmojawapo ya miti ulikuwa na
    kazi yake tofauti:
    - Mti wa sumu,
    - Mti wa mauaji, - Mti wa kutaja/kuonyesha, na
    - Mti kwa ajili ya tiba.
    Alinipa nguvu ya kujibadili katika kila aina ya
    mnyama wa baharini kama
    kiboko, boa constrictor(Nyoka) na
    mamba na kisha akatoweka kabisa. Nilikaa katika bahari kwa wiki nzima kwa
    njia (kama ya mamba) aliyetajwa
    hapo juu nikarudi tena duniani.
    *Maabara za ulimwengu wa chini*
    Nilikaa Lagos kwa wiki moja nikarudi baharini,
    wakati huu nilikaa kwa miezi miwili. Nilikwenda katika maabara
    za kisayansi kuona nini kilichokuwa kinatokea.
    Nikaona madakitari wa akili
    na wanasayansi wanafanya kazi kwa
    umakini sana. Kazi ya wanasayansi hawa ni
    kubuni mambo mazuri kama magari ya kifahari, nk, silaha mpya na
    kujua siri za dunia hii. Na kama ingewezekana
    kujua nguzo ya dunia
    wanayoitaka, lakini Namshukuru Mungu,
    MUNGU TU ANAYEJUA.
    Niliingia katika chumba cha kubuni na huko nikaona sampuli nyingi za nguo,
    manukato na aina mbalimbali za
    bidhaa za urembo. Mambo haya yote
    kulingana na Shetani ni kwa ajili ya
    kuvuruga mitazamo ya wanaume kutoka
    kwa Mwenyezi Mungu. Niliona pia miundo/ ubunifu tofauti ya umeme, kompyuta
    na kengele. Pia kulikuwa na
    TV ambapo walijua wale waliozaliwa tena
    kuwa Wakristo katika ulimwengu.
    Pale unaweza kuona na
    kutofautisha wale ambao ni waendaji wa kanisani tu na wale ambao ni
    Wakristo halisi.
    Nikatoka katika maabara na kuingia katika
    'chumba cha giza' na 'chumba cha
    kukaushia. Chumba cha giza ni
    mahali ambapo wanaua mwanachama yeyote anayeasi.Wanamuua kwanza kwa
    kuchukua damu ya mtu huyo na
    kisha wanampeleka mtu huyo kwenye chumba
    chenye mashine ambapo itamsaga na
    kuwa unga kisha
    wanachukua unga na kuupeleka katika chumba cha kupakia ambapo wataufunga na
    kuupeleka kwa waganga wa
    kienyeji kwa ajili ya hirizi zao. Kulikuwa na
    mambo mengi ambayo ni vigumu
    kueleza kwa maandishi. Pamoja
    na nguvu yote hii ndani yangu, nilikuwa bado sijahitimu kukutana na
    Lucifer/shetani lakini tu nilikuwa na sifa ya
    kuwa wakala wake. Yote sawa,ila niliridhika
    kwamba mimi sasa nilikuwa na
    nguvu na ninaweza kukabili,
    changamoto na kuharibu vitu kadiri nipendavyo. Je, kunaweza kuwa na nguvu
    nyingine yoyote ile popote pale
    basi niliiweka katika mawazo yangu.
    ------------------------------
    *Page 11*
    11 *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    *Sura3: Utawala wa uovu*
    *« Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu;
    mimi nalikuja ili wawe na
    uzima, kisha wawe nao tele.» Yohana * *10:10*
    Nilipokuwa nikirudi Lagos, niliendelea na
    biashara yangu na baada ya wiki
    mbili nikarudi tena baharini. Malkia
    wa Pwani alinipa kile alichokiita "kazi yake ya
    kwanza". Nilitakiwa niende kijijini kwangu na kumuua mjomba
    wangu, mzee mmoja mganga maarufu
    aliyehusika kwa kifo cha wazazi wangu
    kulingana na taarifa yake huyo
    Malkia.
    Nilimtii na nikaenda lakini kwa sababu sikuwahi kuua hapo mwanzo, sikuwa na
    ujasiri wa kumuua, badala yake
    nilimuharibia dawa zake na kumuacha akiwa
    hana nguvu. Kwa sababu ya hili
    nililofanya alipoteza wateja wake
    wote mpaka leo hii. Nikarudi kutoa ripoti ya zoezi hilo lakini alikuwa
    hasira nami. Alisema matokeo ya kutokutii
    maelekezo yake ilikuwa ni kifo, lakini kwa
    sababu ya upendo wake kwangu
    atanituma tena nirudi kijijini na kuua
    wazee wawili ambao alisema waliunga mkono suala la mauaji ya wazazi wangu.
    Kama hii ndio ilikuwa ni adhabu
    kwa kutotii maelekezo yake au sio, mimi sijui.
    Hata hivyo, nilitii na nikarudi kijijini na 'niliweza'
    kuua watu hawa na
    kupeleka damu yao kwake. Kutokana na kitendo hiki kilichotokea katika mazingira ya
    kutatanisha ya kufa, wazee
    katika kijiji wakaenda kuuliza kwa
    mganga mwingine mwenye nguvu ambae kwa
    kawaida huwa anatuma radi kuchunguza
    muuaji ni nani. Kwa bahatimbaya kwa sabab ya watu hawa,
    nilikutana na mganga kiroho ambapo
    alikuwa akijaribu kuongea
    namapepo na nikamuonya asiseme chochote
    kama alipenda maisha yake. Alitoka
    nje na akawaambia wazee waende nyumbani na kuomba msamaha kwa
    mmoja kati ya watoto wao waliemuuzi
    na hakutaja jina langu.
    Radi aliyoituma ikarudi na ikapiga katikati yao
    na kuua baadhi na kuacha
    wengi wamejeruhiwa. Baada ya tendo hili la kwanza, nguvu ndani yangu ilianza
    kujidhihirisha yenyewe.
    Nilimuumbua msichana yeyote aliyekataa
    kufanya urafiki nami nk.
    *Mkutano wangu na Shetani*
    Nikarudi Lagos. Siku moja, msichana mmoja aliyeitwa NINA alikuja kwangu.
    NINA ambae wazazi wake
    wanatokea Jimbo la Anambra alikuwa mzuri na
    mrembo sana lakini anaishi sana
    katika bahari, yaani ulimwengu
    wa chini ya bahari. Alikuwa ni wakala mkereketwa wa Malkia wa Pwani(Queen
    of the Coast) na alikuwa muovu
    sana. Yeye aliwachukia Wakristo sana na
    alikwenda mwendo mrefu kupambana na
    Ukristo. Mimi nilikutana naye
    kwa mara ya kwanza wakati wa ziara yangu ya baharini ya kwanza. NINA
    alikuja kwa ajili ya kazi ya Malkia wa
    Pwani.
    Tuliondoka mara moja na nilipofika pale chini
    niligundua kuwa tutafanya
    kikao na Lucifer/Shetani. Shetani, katika mkutano huu, alitupa maelekezo
    yafuatayo: Kupambana na waamini na
    sio wasioamini, kwa sababu
    wasioamini hao tayari ni wake. Baada ya
    kusema hayo, mmoja wetu akauliza
    swali: "Kwa nini?" Akasema sababu ni kwamba Mungu alimfukuza nje ya 'mahali"
    pale (alikataa kuita neno'
    Mbinguni 'na katika muda wote katika
    mikutano yetu tuliyofanya pamoja naye
    hakuwahi kutaja neno 'Mbinguni'.
    Badala yake alitumia neno 'mahali pale') kwa sababu ya kiburi, na kwa hiyo *yeye
    hataki Mkristo yeyote afike
    huko (Mbinguni).*
    Pia alituambia kwamba hatupaswi kupambana
    na wanafiki. "Wao ni kama mimi,"
    alisema. Aliendelea na hotuba yake na akasema: "Tunapaswa tu kupambana
    na Wakristo halisi" Kwamba wakati
    wake umekaribia, kwa hiyo
    tunapaswa kupambana kama vile haijawahi
    kutokea na kuhakikisha kwamba
    hakuna anayeingia mahali pale:" Sasa mmoja wetu akasema tumesikia
    kwamba Mungu alimtuma mtu kuwaokoa watu
    warudi kwa Mungu" Shetani
    kisha akauliza: "nani huyo?" mjumbe mmoja
    akajibu "Yesu" na kwa mshangao
    mkubwa, Lucifer akaanguka katika kiti chake. Akapiga kelele kwa mtu huyo
    na akamuonya kamwe asilitaje
    jina hilo kwenye mikutano yetu
    ------------------------------
    *Page 12*
    12 *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    kama anapenda maisha yake. Ni kweli
    kwamba kwa jina la Yesu kila goti
    litapigwa (Flp. 2: 10), ikiwa ni pamoja
    na Shetani. Baada ya tukio hilo akatupa sisi moyo na
    alituambia kwamba tusiwajali "hawa
    wakristo", kwamba yeye Lucifer
    atakuja hivi karibuni kutawala dunia na
    atatupa,sisi mawakala wake, mahali
    bora ili tusihadhirike/tusitaabike sawa na wengine duniani na yeye atatufanya
    sisi watawala. *Aliendelea
    kusema kwa kuwa mwanadamu*
    *anapenda mambo ya kushangaza na ya
    ajabu, ataendelea kutengeneza mambo
    hayo na kuhakikisha* *kwamba mwanadamu hana muda kwa ajili ya
    Mungu wake na kwamba atatumia
    yafuatayo kuharibu*
    *kanisa:*
    1.fedha,
    2.mali, 3.Wanawake.
    Mwishoni mwa hotuba hii akafunga Mkutano.
    Mkutano huo ndio uliokuwa wa
    kwanza kwangu mimi kukutana
    na Shetani. Mingine kadhaa ilifuata baada ya
    mkutano huu. Tulipokuwa tukiondoka, Malkia wa Pwani, ambae
    sasa alionekana katika maumbo mbalimbali,
    alinialika mimi na nyumbani
    mwake. Aliingiza majivu ya binadamu
    pamoja na vitu vingine ndani ya mifupa yangu
    ya miguu yote, jiwe (si jiwe la kawaida) katika kidole changu na
    kitu kingine ndani ya mfupa wa mkono wangu
    wa kulia.
    Kila moja ya vitu hivi ilikuwa na kazi yake. Jiwe
    katika kidole changu
    ilikuwa ni kwa ajili ya kujua mawazo ya mtu yeyote dhidi yangu. Moja katika mkono
    wangu wa kulia ilikuwa
    kuniwezesha mimi kuharibu na yale yalio
    katika miguu ni kwa ajili ya kufanya miguu
    yangu kuwa migumu zaidi na
    kuifanya kuwa hatari zaidi na pia kuniwezesha mimi kubadilika na kuwa
    mwanamke, mnyama, ndege, paka, nk
    Alinichukua mpaka kwenye moja
    ya maabara na akanipa darubini, TV na video.
    Hivi havikuwa vitu vya kawaida
    lakini vilikuwa vinatumika katika kuchunguza Wakristo waliozaliwa mara ya pili
    na waendaji tu wa kanisani
    ndani ya kanisa.
    Mwishowe alinipa wasichana kumi na sita wa
    kufanya nao kazi. NINA alikuwa
    ni mmoja wao. Nilikuja tena Lagos nikiwa na zawadi hizo nilizozitaja hapo
    juu.
    *Kugeuzwa kuwa wakala wa shetani*
    Sikuwa na hisia za kibinadamu wala huruma
    katika moyo wangu tena.
    Nilikwenda katika utekelezaji mara moja na niliharibu majengo matano kwa mpigo. Zote
    zilizama ndani ya ardhi na
    wenyeji wao. Hii ilitokea Lagos mwaka
    Agosti 1982. Mkandarasi aliwajibika kwa
    kutoweka msingi mzuri na alilipa
    haswa kwa hili. Uharibifu mwingi unaotokea hivi leo katika dunia si kwamba
    wote umesababishwa na mwanadamu.
    Wajibu wa shetani ni kuiba,
    kuua na kuharibu. Nasema tena, "Shetani hana
    zawadi ya bure".
    Nilikwenda kusababisha ajali katika barabara n.k. Kisa ninachopenda
    kusimulia ni kuhusu kijana mmoja
    aliyekuwa ndio ameokoka tu ambae alikwenda
    akishuhudia wokovu wake na
    ukombozi alioupata. Alikuwa
    anasababisha madhara mengi katika ulimwengu wa roho kwa ajili ya kufanya
    hivi, hivyo nilipanga kufanya ajali
    kwa ajili yake. Siku moja alikuwa kwenye basi
    zuri sana akienda Lagos.
    Alikuwa ameitwa ili aje kutoa ushuhuda
    wake. Basi lilipokuwa katika mwendo wa kasi, mimi nikalizungusha tairi nje
    ya barabara hivyo likaenda na
    kugonga kwenye mti. Abiria wote walikufa
    isipokuwa huyu kijana.
    Kupona kwake ilikuwa ni kimuujiza kwa
    sababu alitoka nje ya gari kupitia buti ya basi na kupiga kelele: "niko
    salama! niko salama! "Tulijaribu kumzuia
    asishuhudie lakini tulishindwa.
    Kwa njia ya TV, tunaweza kujua mtu
    aliyetubu, mpya na tunamfuatilia kwa
    ukaribu kuona kama tunaweza kumfanya akarudi nyuma. Kama baada ya
    miezi sita hatuwezi kufanikiwa,
    tunakwenda katika biashara yake na
    ------------------------------
    *Page 13*
    13 *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    kuifanya iwe mufilisi. Kama yeye ni mtumishi
    wa umma tutamnyanyasa kupitia
    kwa bosi, na kama inawezekana
    tunafanya bosi kusitisha mkataba au uteuzi wake. Kama baada ya haya yote
    hawezi kurudi nyuma basi tunaachana
    nae. Lakini kama atarudi nyuma anauawa
    kuhakikisha kwamba hapati nafasi ya
    pili kutubu.
    Niliharibu maisha kwa kiasi kwamba Lucifer akafurahishwa na kunifanya niwe
    mwenyekiti wa wachawi.
    Mwezi mmoja baada ya Uenyekiti wangu,
    mkutano uliitishwa. Tulihudhuria
    mkutano huo kama ndege, paka na
    nyoka. Viumbe hawa hutumiwa kwa ajili ya sababu zifuatazo:
    1. Kuwa ndege kunafanya wachawi wawe
    hatari zaidi.
    2. Kuwa paka kunafanya wachawi wawe na
    uwezo wa kuwa katika roho na
    binadamu. 3. Kuwa panya kunawawezesha wachawi
    kuingia katika nyumba kwa urahisi,
    kisha wakati wa usiku wanakuwa
    kivuli, na kisha binadamu na kunyonya damu
    za watu.
    Katika mkutano huo tulikuwa na agenda moja tu: *"Wakristo" *Tukapanga
    kuitisha mkutano wa Afrika wa
    wachawi mjini Benin mwaka 1983.
    Tulichapisha katika magazeti yote ya kila
    siku na vyombo vyote vya habari
    vya umma. Nguvu zote za giza walijipanga na walikuwa na uhakika sana kwamba
    hakuna kitu chochote
    kitakachoingilia kwa kupinga mkutano huu.
    Kwa kweli kila kitu kilipangwa
    vizuri na kulikuwa hakuna mwanya.
    Ghafla, Wakristo Nigeria wakaingia kwenye maombi na sifa kwa Mungu wao na
    mipango yetu yote ilizimwa. Si
    tu kwamba mipango yetu ilizimwa peke yake
    lakini pia kulikuwa na mtafaruku
    haswaa katika ufalme wa giza.
    Matokeo yake, mkutano wa wachawi 'na mapepo haukuweza kufanyika Nigeria.
    Wakristo wanapaswa kutambua
    kwamba wakati wao wanaingia ndani katika
    sifa halisi kwa Mwenyezi Mungu,
    kunakuwa na shida na mvurugano
    kote ndani ya bahari na angani,na mawakala wa shetani wanakuwa hawana
    nafasi ya kupumzika/kutulia. Maombi
    ni kama kutupa bomu la kushitukiza katikati
    yetu na kila mtu anatoroka
    kuokoa maisha yake.
    Kama Wakristo wakitambua na kutumia nguvu na mamlaka ya Mungu aliyowapa,
    wataweza kudhibiti mambo
    ya taifa lao! Wakristo tu ndio wanaonaweza
    kuokoa taifa letu.
    Baada ya mkutano huu kushindikana, ambao
    baadae ulifanyika nchini Afrika Kusini, niliitwa tena baharini.
    Nilipofika, niliambiwa kutokea wakati huo
    nilitakiwa kufanya bahari kama
    nyumbani kwangu na kutembelea
    dunia kwa shughuli ngumu tu. Nilipewa kazi
    mpya: kubuni hirizi za waganga, nikiwa mhusika mkuu wa chumba
    na mtumaji wa zawadi, yaani ufunguzi wa
    makanisa (nyumba za maombezi),
    ufunguzi wa nyumba za kujifungua,
    kufungua maduka na kufanya yafanikiwe,
    kuwapa 'watoto na fedha. Haya yataelezwa moja baada ya jingine:
    *1. Ufunguzi wa "Makanisa ya nguo nyeupe":*
    Wakati mtu anakuja kwetu kwa msaada wa
    kujenga nyumba ya maombi na
    kumsaidia kufanya uponyaji nk,
    basi atapewa baadhi ya sheria: a) Atakubali kuchangia kwetu nafsi moja au
    mbili kila mwaka.
    b) Katika ngazi fulani ya ofisi katika kanisa mtu
    atakuwa anaunganishwa na
    jamii yetu.
    c) Hakuna mwanachama angeruhusiwa kuja katika nyumba ya maombi na viatu
    mguuni.
    Akisha kubali matakwa hayo,*atapewa kitu
    changarawe nyeupe, mifupa ya
    binadamu, damu na hirizi, vyote*
    *katika chungu*. Atapewa maelekezo ya *kuzika chungu hiki na vitu vyake
    vyote mbele ya kanisa na atazika*
    *msalaba juu yake*. *Baada ya maziko
    msalaba tu ndio unapaswa kuonekana.
    *Atashauriwa
    *kujenga Bwawa* *au kuweka basini ambapo roho chafu
    zinaendelea kuweka maji maalum. Maji
    haya ndiyo unasikia huyaita*
    *"maji matakatifu."*
    Watu wengi wakisumbuliwa na roho mbaya
    wanakwenda kwa hawa "manabii" kwa ajili ya kuwafukuza. Ukweli
    ni kwamba, wao huongeza mapepo zaidi kwao.
    *Shetani hawezi kumuondoa nje
    shetani. *(Luka 11:17-19) Kile
    ------------------------------
    *Page 14* 14
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    nabii atakifanya ni, atamuombea mshirika na
    kisha atampa mshirika kitambaa
    chekundu ili kuweka katika nyumba yake, na kisha atamshauri awe
    anaomba akiwa na mishumaa na uvumba.
    Kwa kitendo hiki mtu anatualika
    sisi kwenye nyumba yake. Wakati mwingine
    mshirika anashauriwa kuleta mbuzi
    n.k, kwa ajili ya sadaka. Sadaka hizi ni kwa ajili yetu kuja na kusaidia kumtibu
    mtu huyu. Nabii hana uwezo
    wa kutibu au kuponya
    *2. Ufunguzi wa Maternities (sehemu za
    kujifungulia):*
    Kama mwanamke anakuja kwetu kwa ajili ya kupata msaada wa kufungua kituo
    cha uzazi na kukifanya
    kifanikiwe, atapewa sheria zifuatazo:
    "Mwezi utachaguliwa ambao watoto wote
    wanaozaliwa katika mwezi huo kwenye
    kituo hicho watakufa, na miezi mingine watoto wataishi."
    Kama atakubali basi atapewa, dawa ambayo
    itawavutia watu kuingia katika
    kituo hicho cha uzazi. Kuna
    maternities kama hizi Onitsha, Lagos, nk viatu
    haviruhusiwi katika vituo hivyo.
    *3. Ufunguzi wa Maduka ya dhana:*
    Mtu anapotufuata sisi kwa ajili ya msaada
    katika suala hili, anapewa pete
    na mashariti kwamba hakuna
    mwanamke atakayeruhusiwa kugusa pete yake. Ni lazima pia akubali kuwa
    mwanachama wetu. Kama atakubali
    kupokea kutimiza masharti hayo, duka lake
    litakuwa linajaa vifaa vya ubora
    na vya kisasa.
    *4. Kutoa Watoto* Kama mwanamke tasa atakwenda kwa
    mganga, baada ya kuweka malalamiko yake,
    ataulizwa kuleta yafuatayo:
    jogoo mweupe, mbuzi, chaki ya asili na baby
    care. Ataambiwa arudi na
    atakapokuwa ameondoka,mganga atakuja kwetu kuleta vitu hivi. Kisha
    tutachanganya vitu fulani ambavyo ni
    vigumu kuelezea kwa maandishi, na
    tutaweka majivu ya mwanadamu. Atatumia
    dawa hii kumpikia chakula mwanamke
    nk. Atapata mimba na kuzaa, lakini siyo binadamu wa kawaida. Kama
    mtoto ni wa kike ataweza
    kuishi na hata kuolewa lakini
    atakuwa bado tasa maisha yake yote. Kama
    mtoto ni wa kiume ataishi lakini
    atakufa kifo cha ghafla. Huwa awaishi kuzika wazazi wao.
    Napenda kukueleza hapa kwamba utasa mara
    nyingi unasababishwa na mapepo.
    Unaweza kuona mwanamke
    tasa hapa duniani, lakini anaweza kuwa na
    watoto wengi tu baharini. Kwa hiyo nashauri watoto wa Mungu
    kumsubiri Mungu pekee kwa sababu Mungu tu
    ndio huwapa watu watoto halisi.
    *5. Kutoa fedha:*
    Kama mtu anakuja kwetu kwa ajili ya kupata
    fedha, atapewa masharti yafuatayo kuyatimiza: Ataambiwa kutoa
    sehemu ya mwili wake au kama ana familia
    ataambiwa kuleta mtoto wake wa
    kiume. Kama yuko mwenyewe
    basi ataombwa kumtoa kafara kaka yake au
    mdogo wake. Yeyote atakayeamua kumleta ni lazima atoke
    katika tumbo moja. Kitu muhimu
    cha kutaja: siku ya kufanya
    mauaji ya mhusika, mtu ambaye amempeleka
    atapewa mkuki,au mshale. Uhusiano
    wake utawekwa katika file kwenye kioo. Mara baada ya mtu yule
    anayetakiwa kumtoa kupita, ataambiwa
    apige ile sehemu ya faili iliyo
    kwenye kioo,basi akifanya tu hivi yule mtu
    anakufa pale mahali alipo.
    Kuna njia nyingine lakini jambo moja Shetani hufanya ni kwamba:
    anahakikisha kwamba katika njia hio
    tofauti, mtoaji anakuwa mwajibikaji kwa ajili ya
    kifo cha mwathirika, kwa
    kufanya mtoaji ampige mlengwa,
    kumbuka *Shetani hana zawadi ya bure!* ------------------------------
    *Page 15*
    15
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    *Sura 4: Jinsi shetani anavyopigana na Wakristo*
    *«Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya
    damu na nyama; bali ni juu ya
    falme na mamlaka, juu ya wakuu *
    *wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya
    katika ulimwengu wa roho. »* *Waefeso. 6: 10-12 *
    *Kupigana na Wakristo*
    Baada ya amri ya Lucifer kupambana na
    Wakristo, sisi tuliketi na kuchora
    ramani ya kupambana nao kama
    ifuatavyo: 1. Kusababisha magonjwa.
    2. Kusababisha utasa.
    3. Kusababisha usingizi katika kanisa.
    4. Kusababisha machafuko katika kanisa.
    5. Kusababisha uvuguvugu katika kanisa.
    6. Kuwafanya wawe wajinga wa neno la Mungu.
    7. kwa mitindo na uigaji.
    8. Kupambana nao kimwili.
    Miongoni mwa hayo juu napenda kuwaeleza
    mawili:
    *1. Kupambana kimwili:* Kwa TV niliyopewa, niliwaona Wakristo
    waliozaliwa mara ya pili. Hatupigani
    na wanafiki kwa sababu wao ni
    mali yetu tayari. Tuliweza kuwatuma
    wasichana wetu kwanza katika makanisa
    makubwa. Ndani ya kanisa walikuwa wanatafuna jojo au kumfanya mtoto
    alie au kufanya chochote ambacho
    kilivuruga watu kusikiliza neno
    la Mungu. Wanaweza kuamua kuja kiroho na
    kusababisha watu kulala wakati
    mahubiri yanaendelea. Wakikuona uko makini kwa sababu ya mahubiri,
    wanaweza kukusubiri nje ya kanisa na
    unapokuwa ukitoka kuja nje ya
    kanisa, mmoja wao anakusalimu na hata
    kukupa zawadi ( na mara nyingi ni
    zawadi ya kitu kile upendacho ) na wataonekana ni marafiki sana. Atafanya
    kila kitu na kabla haujajua
    kinatokea unakuwa umesahau kila kitu
    ulichojifunza kanisani . Lakini kwa Mkristo
    halisi,mmoja ya wasichana hawa
    ,baada ya ibada, ataruka nje kukusalimu na atapenda kujua nyumba yako
    kwa kisingizio kwamba yeye ni
    mgeni katika mji na hawajui
    Wakristo wengi wanaomzunguka. Ukimpeleka
    nyumbani kwako, kwa haraka
    atanunua ndizi na Mkristo atachukulia hii kama ishara ya upendo.
    Ataendeleza ziara zake mpaka
    hatimaye anaweka mbali mwanga wa
    Kristo ndani yako na kisha anaacha kuja.
    Shughuli kuu katika makanisa
    yaliyo hai na shirika zilizo hai ni : kuwasumbua Wakristo wasisome na kujifunza
    neno la Mungu, na hivyo kuwafanya
    wajinga wa mamlaka na
    ahadi za Mungu. Katika mikutano ya injili
    wasichana hawa wanatumwa
    kusababisha kutoelewana na ugomvi. *Jinsi wakirsto wanavyojulikana?*
    Wakristo waliozaliwa mara ya pili hawajulikani
    kwa Biblia wanayobeba kila
    siku au ibada nyingi
    wanazohudhuria. Wanajulikana katika
    ulimwengu wa roho kwa mwanga ambao huendelea kuangaza wakati wote
    kama mshumaa mkali sana katika moyo au
    mduara wa mwanga unaozunguka kichwa
    au ukuta wa moto
    unaowazunguka. Mkristo anapokuwa
    akitembea, tunaona malaika wakitembea pamoja naye mmoja mkono wa
    kuume, mmoja kushoto, na mmoja nyuma. Hii
    inafanya kuwa vigumu kwa sisi
    kuja karibu yake.
    Njia pekee ya sisi kufanikiwa ni kwa kumfanya
    Mkristo atende dhambi, na hivyo anatoa mwanya wasisi kuja na
    kuingia ndani. Mkristo akiwa anaendesha gari
    na tunapotaka kumdhuru,
    tunaona kwamba siku zote hayuko peke
    ------------------------------
    *Page 16* 16
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    yake katika gari. Siku zote kuna malaika
    pembeni mwake. *Oh kama Mkristo
    akijua tu yote ambayo Mungu* *anafanya kwa ajili yake, hawezi kutenda
    dhambi au kuishi ovyo ovyo !*
    *2. The Making of Backslidden Christians*
    Kama mwenyekiti aliyeteuliwa na Lucifer,
    niliwatuma wasichana hawa
    makanisani na sharika zinazoishi/hai . Wasichana hawa wanakuwa wamevalia vizuri
    na baada ya mahubiri wanakuja
    kwenye madhabahu kama
    wameitwa, na watajifanya kuwa wamempokea
    Kristo na wataombewa. Mwishoni mwa
    ushirika au ibada watazungukazunguka nje na kumsubiri
    mhubiri ambaye kiukweli atakuwa na
    furaha sana na waongofu hawa
    wapya.
    Waongofu hawa wapya wanaweza hata
    kumfuata mhubiri nyumbani kwake. Kama mhubiri hana roho ya
    kupambanua watamvutia aingie katika dhambi
    ya uzinzi au uasherati . Hii
    inafanyika wakati pale mhubiri
    anapokuwa amemtamani. Atahakikisha
    amendelea katika dhambi hii mpaka pale atakapoona amemzimisha Roho
    wa Mungu ndani yake na kisha anaondoka,
    huku *mkakati wake umetimia.*
    Mahali hapa ningependa kutoa ushuhuda wa
    Mhubiri. Katika ulimwengu wa
    roho/kipepo yeye anajulikana kama mtu wa Mungu(man of God). Anapokwenda
    kwenye magoti yake kunakuwa na
    mvurugano kati yetu. Kwa hiyo
    tunatuma wasichana hawa kwake. Mtu huyu
    anaweza hata kuwalisha lakini
    atakataa kunaswa na mitego yao. Walijaribu kila walivyoweza lakini kamwe
    hawakuwahifanikiwa. Matokeo
    yake, wasichana hawa waliuawa
    kwa kushindwa kwao.
    Mimi nilijigeuza na kuwa mwanamke kisha
    nikamwendea, kwa maneno na vitendo nilijaribu kumshawishi, lakini
    alikuwa mgumu. Hii ilikuwa ni kazi kubwa mno
    kwangu, hivyo nilidhamiria
    kumuua kabisa kimwili. Siku moja,
    Mhubiri huyu alikwenda soko la barabara ya
    Oduekpe. Nilimwangalia na alipoinama chini kununua baadhi ya
    bidhaa nilijizungusha kwenye tairi za trailer
    iliyokuwa imebeba mafuta ya
    mafuta kuelekea sokoni alipokuwa
    mhubiri. Trailer/gari likapiga nguzo kubwa sana
    ya NEPA na ikangukia katikati ya soko, na kuacha watu wengi
    wamekufa, lakini Mhubiri alitoka mzima. Jinsi
    gani alipona ulikuwa ni
    muujiza. Siku nyingine, nilimuona
    akisafiri kwenda Nkpor kwa miguu.
    Nililizungusha gari la jeshi lililokuwa limebeba viazi vikuu vya kumuua.
    Lori lilikwenda moja kwa moja ndani ya
    barabara mpya ya makaburini, na
    kuwaua watu wengi mno, lakini
    muhubiri huyu bado alikuwa mzima. Baada ya
    jaribio hili la pili tulikata tamaa.Yeye bado yuko hai hata leo hivi!
    Kwa sababu ya mkristo mmoja, shetani
    anaweza kuamua kuharibu roho nyingi,
    akifikiri anaweza kumuua, lakini
    siku zote anashindwa. Matukio haya
    yameyotokea kwa Wakristo wengi bila ya wao kujua, lakini Mungu wao
    huwaokoa mikononi mwa adui zao siku zote.
    Shida ni kwamba, Shetani hachoki.
    Mawazo yake yako palepale:
    "Ninaweza kufanikiwa." Lakini kamwe
    hafanyikiwi. kama tu Mkristo atatembea na *Upendo wa Mungu na *
    *kubakia ndani yake na ajichanganyi na
    mambo mengine ya maisha haya,
    shetani hawezi kumpata,*
    *vyovyote vile shetani anaweza kujaribu.
    Wasioamini tu ndio wako chini yake.*
    *Ukandamizaji wa Wakristo*
    Hii hutokea hasahasa katika ndoto. Mkristo
    anaweza kuona katika ndoto yake
    yafuatayo:
    1. Mtu mfu anamtembelea 2. Kinyago kinamfuata.
    3. Marafiki wanaogelea katika mto
    4. Marafiki wanaleta chakula na wanamsihi ale.
    5. Msichana wa kike anafanya ngono au
    msichana aliyeolewa anafanya mapenzi
    na mwanaume. Hii, kama si haitashughulikiwa, wakati mwingine
    husababisha utasa.
    Au mwanamke mjamzito anajiona anajamiiana
    na mtu. Hii, kama
    haikushughulikiwa, inaweza kusababisha
    kuharibika kwa mimba. ------------------------------
    *Page 17*
    17
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    Kama Mkristo akikutana na hayo huu katika ndoto yake, hatakiwi kuweka kando
    mambo haya kwa kupuuzia
    bali akitoka kwenye ndoto tu inampasa
    ajichunguze mwenyewe na atubu dhambi
    yeyote ile inayojulikana na
    kufunga pepo wote na kumsihi Mungu arejeshe kila kitu alichokutana nacho
    ndotoni. Hii ni muhimu sana. Mtu
    ni lazima pia kutafuta msaada na ushauri kwa
    mkristo aliyejazwa na Roho
    Mtakatifu, wakongwe katika imani.
    *Shetani na mkakati wa kuvuna roho* Yesu Kristo alipokuwa akiondoka duniani,
    aliwapa wanafunzi wake amri:
    "Akawaambia enendeni ulimwenguni
    kote mkafanye wanafunzi kwa kila taifa"
    Wakati Wakristo bado wanasubiri
    mazingira mazuri na wakati mzuri kwa ajili ya kutii amri hii, Tofauti ni kwamba,
    *mawakala wa shetani wako
    na bidii kubwa zaidi katika kuvuna*
    *roho za Wakristo !*
    Moja ya maeneo ya shetani katika kuvuna
    roho ni shule za sekondari, hasa za wasichana. Baadhi ya wasichana
    wetu wanatumwa katika shule kama
    wanafunzi. Tunawapa kila chupi ya kisasa
    na nzuri na zenye gharama kubwa.
    Hii ndio kipaumbele cha kwanza, kwa sababu
    katika hosteli za wasichana wao hupendelea kutumia chupi tu .
    Mawakala wetu kamwe hawakosi kitu
    chochote, vipodozi, nguo , chupi ,
    vitabu, fedha na mahitaji. Sabuni
    maalumu za kuoga atapewa ili kutoa kwa
    mwanafunzi yeyote ambaye atahitaji sabuni kutoka kwake. Msichana
    anayetaka kuwa kama yeye atavutiwa na
    kufanya urafiki nae. Hatua kwa hatua
    wakala wetu atatutambulisha
    kwake. Nasi tutamtembelea kimwili na kuanza
    kumpa zawadi na kumtimizia mahitaji yake. Kwa hili, atajiunga
    nasi kwa hiari . Yeye naye atawavuta wengine
    na itaendelea hivyo. Hii
    inachukuliwa kama mkakati wenye
    dhamira ya kufanikiwa.
    Jambo moja la kuzingatia: shetani hamlazimishi mtu yeyote. Anachokifanya ni
    kuwavutia watu na kuwafanya
    waje kwake kwa hiari. Ndiyo maana Biblia
    inasema: "mpingeni shetani naye
    atawakimbia" (James 4:7). Eneo
    jingine la kuvuna roho la shetani ni kutoa lifti. Tunawapeleka wasichana
    wetu kusimama barabarani, na kwa
    kawaida huwa ni warembo sana na wamevaa
    mavazi ya kuvutia. Unaweza pia
    kuwapata kwenye hoteli na kupitia
    maeneo haya tunawapata wanaume na wanawake. *Watu wengi tunaowaona
    wanatangazwa katika magazeti*
    *kama wamepotea, ni baada ya kutoa lifti kwa
    wasichana, wasiowajua.*
    Unapaswa kuwa makini ni nani ambaye
    unampa lifti. ------------------------------
    *Page 18*
    18
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    *Sura 5: Nilipokutana na Yesu* Katika mwezi Februari 1985, tulikuwa na
    mkutano wetu wa kawaida katika
    bahari, baada ya hapo niliamua
    kusafiri kwenda Port Harcourt katika jimbo la
    Rivers, kutembelea mke wa
    marehemu mjomba wangu. Nilikutana na mtu mmoja aitwaye Anthony. Yeye ana
    karakana pale kwenye makutano ya
    Nwaja, sambamba na barabara ya
    Trans-Amadi, Port Harcourt, Rivers State.
    Alimtuma mtu huyu kwa ajili yangu
    na kwa sababu katika jamii yetu tuna sheria kwamba hatupaswi kukataa muito,
    niliamua kujibu muito wake.
    Nilikwenda kwake mchana siku ya
    Alhamisi ya wiki hiyo. Alianza kwa kusema
    Mungu amempa ujumbe kwa ajili
    yangu. Akatoa Biblia yake na kuanza kuhubiri. Kulikuwa na Wakristo
    wengine watatu wameketi (mwanaume na
    wanawake wawili). Aliendelea
    na mahubiri yake kwa muda mrefu na sikuwa
    na uhakika kama nilisikia yote
    aliyosema. Alinisihi nipige magoti kwa ajili ya maombi. Nilimtii na taratibu nikapiga
    magoti.
    *Mara ghafla akaanza maombi yake.
    Naliangushwa chini na roho wa Mungu na
    nikaanguka*
    *nikajinyoosha*. Nilijitahidi kuinuka na nikasimama kama chuma.
    Nikavunjavunja viti vya chuma ndani ya
    karakana. Niliangalia nje na kuona
    wanachama watatu wa jamii yetu ya siri,
    mwanaume na wasichana wawili.
    *Walikuja katika umbo la binadamu na kusogea mpaka mlangoni lakini kwa
    sababu ya nguvu ya Mungu*
    *hawakuweza kuingia.*
    Nina hakika kengele ndani ya bahari
    iliwataarifu shida ilipokuwa na kwa TV
    walijua wapi ambapo tatizo lilikuwa na walituma waokoaji wasio na nguvu. Hii
    mara zote hufanyika wakati
    mwanachama yeyote ameingia katika
    matatizo. Wakati wale wakristo wawili
    wakinivuta chini kwenye magoti yangu,
    wasichana wawili waliendelea kuomba na kufunga mapepo, lakini hawakuwa
    wanalenga hasa nini wanachofunga.
    Wakaniuliza kama
    ninamuamini Yesu Kristo, sikusema chochote.
    Wakaniuliza niite jina la Yesu,
    nami nilikataa. Wakaniuliza jina langu niliwaambia. Wakajitahidi kwa masaa na
    wakaniachia niende. Hakuna
    roho iliyoondolewa ndani mwangu,
    hivyo nilitoka hivyohivyo sawa na nilivyoingia.
    *Maatukio ya Kanisani*
    Siku iliyofuata ilikuwa ni Ijumaa, nilialikwa na Anthony huyo huyo
    kuhudhuria usiku wa mkesha wao katika
    kanisa la Assemblies of God, Silver Valley,
    Port Harcourt. Nilikubali
    mwaliko huu kwa sababu kuhudhuria ibada
    ya makanisa na kusababisha usingizi na machafuko ilikuwa ni sehemu ya kazi
    yetu. Ibada ilianza na pambio.
    Tuliimba mpaka mmoja wa wajumbe
    wenzangu akaanzisha kiitikio maarufu cha
    bendi moja ya kikristo,
    kinachozomea uwezo na mamlaka ya nguvu zingine isipokuwa nguvu za Yesu.
    Kisha nikaanza kucheka. Nilicheka kwa
    sababu katika roho niliwaona maisha
    yao karibu robo tatu ya watu
    waliokuwa wanaimba kiitikio kile walikuwa
    wanaishi katika dhambi. Nilijua kuwa *kwa sababu ya dhambi*
    *katika maisha yao, ni wazi kuwa
    wangeharibiwa vibaya na nguvu hizi. Ni
    muhimu kwa wakristo kutii neno*
    *la Mungu na si kuruhusu dhambi kubaki katika
    maisha yao. *Katika ibada hiyo tulikuwa wanne kutoka
    baharini na tulikuwa tukiimba na kupiga makofi
    pamoja nao. Tena nataka
    kusisitiza hapa kwamba wakati ibada
    inaanza, waumini ni vyema na wanashauriwa
    kwanza kukiri dhambi zao na kutubu, kisha kwenda katika kipindi
    cha sifa halisi kwa Mungu. Hii itafanya wakala
    wa Shetani awe na wasiwasi
    sana na ataondoka ili kuyaokoa
    maisha yake.
    Katika ibada hii tulikuwa tunaujasiri sana hata tukaingia katika utendaji.
    Wengi walianza kulala, pambio zilikuwa
    zikiimbwa kwa udhaifu na mambo yakaenda
    zig-zag. Ndugu Anthony alikuwa
    tayari amewaambia kuhusu mimi
    kwa hiyo saa 02:00 waliniita nitoke mbele na waanze kuniombea. Mara
    nilipotoka mbele walianza kuita damu ya
    Yesu. Nikawasimamisha na kusema: "Si
    kuomba kwa damu ya Yesu ndio ufumbuzi.
    Mimi ni mwanachama
    mkubwa sana katika jamii za watu wa chini ya bahari. Kama mnakubali kwamba
    mnaweza kunikomboa, basi
    nipige magoti. "Maneno haya niliyasema
    sikuwa nimeyapanga. *Damu ya Yesu
    inaogopesha mapepo na *
    ------------------------------ *Page 19*
    19
    *Imefasiriwa na Peter Kahale kwa Neema
    aliojaliwa na Mungu*
    *kumlinda muamini, lakini haifungi mapepo.
    Kufunga mapepo na kuyatoa inafanyika tu pale Mkristo*
    *anapotumia mamlaka yake na kutoa amri.*
    Walikubaliana na mimi nikapiga magoti. Katika
    hatua hiyo dada mmoja
    aliiongozwa na Roho wa Mungu na
    kuongea kwa sauti akasema: "Kama hauko vizuri, usijaribu kusogea karibu!"
    Nina uhakika wengi hawakuwa
    wameelewa nini maana yake. *Ni hatari kwa
    Mkristo anayeishi katika dhambi
    kutoa pepo. *Wengi waliondoka
    na wachache wakatoka kuja kuomba kwa ajili yangu. Walipoanza kusema "Katika
    jina la Yesu," Nikasikia
    (mpasuko mkubwa) big bang kubwa ndani
    yangu na nikaanguka juu ya sakafu.
    Mara pepo wanaokuruka ndani
    yangu wakanza kufanya kazi. Nikaanza kukimbia kwa kifua changu. Mtu yeyote
    mwenye hili pepo la kuruka ni
    muovu na hatari sana. Ndugu/Waamini
    hawakuona nini kinatokea kiroho.
    Nilikuwa nakimbia mbio kwa sababu
    ya nguvu kubwa iliyokuwepo katika chumba. Nguvu mbili za upinzani zikaanza kufanya kazi
    pia na anga likabadilika.
    Ghafla nikasimama na nikawa na vurugu
    sana nk. Pepo, likatoka ndani yangu na
    kumkamata mvulana aliyekuwa kati yao
    na likaanza kupambana nao, likijaribu kuniokoa mimi. Ndugu hawakupoteza
    muda nae badala yake
    wakamkamata yeye pamoja na wengine
    waliokuwa wanaogopa na kumfungia katika
    vestry ya kanisa. Hii iliendelea
    mpaka 7:00 Nilikuwa nimechoka sana kimwili na nikawa nimetulia, hivyo ndugu
    wakakusanyika karibu yangu
    tena na kuanza kuniambia: Wataje
    ni akina nani hao nk Nilikaa kimya tu. Baada ya
    kusubiri kwa muda mrefu na
    kuona sikuwa nimesema kitu, walidanganyika na kuamini kwamba nilikuwa
    nimekombolewa. Wakaomba na
    tukatawanyika. Nilikuwa kimwili
    dhaifu kiasi kwamba ilikuwa ni vigumu
    kutembea kwenda hata nje ya kanisa.
    Lakini kitu fulani kilitokea, mara baada ya kwenda nje ya kanisa na kuvuka
    barabara, nikawa na nguvu nyingi za
    kimwili. Labda inawezekana baadhi ya mapepo
    yaliyotoka yakarudi tena ndani
    yangu. Nilikasirika sana na
    kuamua kulipiza kisasi juu ya kanisa. "Hawa watu wamenidhalilisha"
    Nikajisemea mwenyewe, na kwa jinsi
    walivyonifanyia nitarejea Lagos na kupata
    nguvu zaidi pamoja na wengine
    waovu kama mimi, na kisha narudi
    Port Harcourt kulipiza kisasi kwa kanisa zima la Assembly of God, Silver
    Valley.
    *Safari yangu ya Lagos*
    Nilipofika kwenye nyumba ya mke wa mjomba
    wangu, Niliwaambia nitaondoka
    kurudi Lagos mara moja. Nilikataa wasinisihi kubaki na nikachukua teksi
    mpaka kituo cha magari cha
    Mile 3. Ambapo nilichukua teksi
    ya kwenda Onitsha. Nia yangu ilikuwa
    kusimama Onitsha, kumuona rafiki na
    kisha kuendelea mpaka Lagos. Pale Mile 3 tukaondoka na tulipokuwa tumefika njia
    panda ya kwenda Omagwe,
    katika makutano ya uwanja wa ndege
    wa Kimataifa, nikasikia sauti ikiniita kwa jina
    langu la asili "NKEM."
    Nikageuka nyuma kuona kama kuna sura yeyote ninayoijua kwenye teksi, lakini
    hakukuwa na mmojawapo anayenijua.
    Huyu anaweza kuwa nani? Ni
    marehemu mama yangu tu ndiyo alikuwa
    akiniita kwa jina hilo, wengine wote
    pamoja na ulimwengu wa kipepo walinijua mimi kama Emmanuel.
    Nilipokuwa bado nashangaa, sauti ikasikika
    tena : *" NKEM , unakwenda
    kunisaliti kwa mara nyingine tena *
    *?" *Sikuweza kuitambua sauti lakini sauti
    iliendelea kuniuliza : *" Je, unakwenda kunisaliti kwa mara nyingine*
    *tena*" Ghafla nikawa na homa kali. Joto
    lililotoka mwilini mwangu lilikuwa
    liko juu mno kiasi kwamba abiria
    wengine walilisikia. Mmoja wao akaniuliza:
    "Mheshimiwa, ulikuwa vizuri kabla ya kusafiri?"Niliwaambia
    nilikuwa vizuri na sikuwa naumwa hata na
    kichwa kabla ya kuondoka Port
    Harcourt.
    Tulipofika Umuakpa Owerri, nilianguka ndani
    ya teksi. Kilichofuata ni kwamba watu wawili, warefu na
    wakubwa, walikuja kunichukua mmoja upande
    wa kushoto na mwingine upande wa
    kuume, na hawakuzungumza
    neno lolote kwangu. Waliniongoza kwenye
    barabara mbaya sana yenye chupa na vipande vya chuma vilivyokuwa
    vinanikatakata nikaanza kulia, lakini hawa watu
    hawakusema neno lolote.
    Tuliendelea mbele na kufika kwenye
    barabara ya kasi. Ilikuwa hapa mmoja
    akaniambia *"Wewe unatafutwa sana"*na tukaendelea. Tuliendelea mpaka
    ------------------------------

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate