Wafilipi 2:10-11
  • UJUMBE KUTOKA KWA BWANA YESU KWAAJILI YA MATAIFA YOTE

    Umeandikwa na Dkt. Augostino Maquengo* *Ulipokewa na Dkt. Augostino Maquengo
    mnamo tarehe 16/5/11:* www.DivineRevelations.info/SWAHILI <http://www.divinerevelations.info/SWAHILI > Bwana alinitembelea asubuhi mara tu nilipofika
    ofisini. Niliuhisi uwepo
    Wake kisha mkono
    ukanijia juu ya mabega yangu.Nami nilihisi
    moto juu yangu na nikaisikia
    sauti ya Bwana ikiniongelesha akisema: " yaandike chini na
    uwaambie."
    Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi
    Mungu
    kwa wachungaji, wainjilisti, makasisi na
    watumishi wengine: " ghadhabu yangu itawamaliza" Nanyi hamtanyakuliwa,
    kwani mmeziacha
    njia zangu na kuwafanya kondoo wangu mali
    yenu binafsi na chanzo cha
    utajiri wenu ,Kwa hiyo
    Bwana hatawanyakua wachungaji hawa,wanjilisti na watumishi wangu waliopenda
    ufanisi badala
    ya ujumbe wa kutubu,kubadilika, kuja kwangu
    ambako kuko karibu na mada ya
    kunyakuliwa.
    Kanisa wanalolisema kuwa langu, limekuwa ukumbi wa kujitumbuiza likiongozwa
    na
    wachungaji,makasisi na mashemasi wa
    kanisa. Wala na kunywa na kusherehekea
    nyumbani
    mwangu na mbele yangu pasina kuogopa,kutetemeka au kuniheshimu. Oh,
    Utukufu
    Wangu
    umeondoka mahekaluni mwao na uwepo
    Wangu uliondoka kitambo kutoka
    makanisani mwao. Wao hawatanyakuliwa wasiponililia mimi
    Mungu wao kwa uchungu katika toba.
    Watumishi wangu wamepotoshwa na
    ulimwengu nao sasa wanafanya mipango ya
    kuingiza njia za
    kiulimwengu makanisani. Wao husherehekea siku ya wapendanao kanisani na pia
    husherehekea
    siku ya kimataifa ya waongo kanisani ,nao
    husema katika siku ya kuomboleza
    ,leo ni siku ya
    majonzi nasi basi tuvalie mavazi meusi. Wote wamepotoshwa.
    Wachungaji,wainjilisti na makasisi wametabiri
    nyakati za utele,nyakati za
    kukombolewa na
    kufanikiwa ilhali panakuja humu ulimwenguni
    misiba na mateso makubwa, na kuharibiwa kwa
    ulimwengu. Watumishi wangu hawanisikii
    kamwe.
    Wamejipotosha na ulimwengu na hata
    wameziacha njia zangu.
    Wao hawanitafuti katika maombi ,kufunga na kulitafkari neno langu. Wao
    hufunga na kuomba ili
    kuniomba vipawa vya kuponya,miujiza na
    kutabiri kwa manufaa yao wenyewe. Na
    hata wao
    husema: Nitatayarisha ujumbe wa kuhubiri. Nitatayarisha mkutano. Mimi nina
    shughuli nyingi ya
    kuwapa ushauri nasaha waumini.lazima
    niwatunze waumini, nao hawana wakati
    kwa ajili yangu
    Mimi, ambaye ndiye mmiliki wa kondoo hawa. Hawa wachungaji hawatanyakuliwa
    asema Bwana
    wa majeshi. Ikiwa hamniogopi mimi, basi
    zirarueni nguo zenu,nyoyo zenu na
    hata akili zenu kwa
    machozi na kutubu. Nataka toba la kitaifa la kanisa ,maombolezo na kilio.
    Mjivishe mavazi ya
    vumbi na mlie kwa toba la sivyo nyinyi
    hamtakuja kwangu mbinguni.
    ------------------------------
    *Page 2* 2
    Kondoo wangu wanakula chakula kilicho
    oza,kilichorogwa kutokana na jumbe za
    watumishi
    Wangu na hawa wachungaji.
    Wanaekeza kwa ajili ya siku za usoni kwa miradi ya ujenzi kanisani nao
    hawafahamu kwamba hii
    miradi yote itakatizwa na maangamizo na
    majangwa ya ghafla. Baada ya
    kuliokoa kanisa langu
    kutoka humu ulimwenguni,hii miradi yote ya ujenzi itageuzwa kuwa bure. Ni
    viwekezo ambavyo
    havita zaa chochote.
    Badala yake yafaa muwekeze katika kuhubiri
    neno la uhai lisilo bandia.
    Hubirini badala yake Kufanikiwa kwa nafsi na roho kupitia kwa toba
    na uzima wa milele. Bwana
    asema hivi, nalipenda
    sana kanisa langu,ambalo hunitafuta kila siku
    na huliogopa jina langu
    takatifu!! Wakati umekwisha. Wakati umefika tamati.
    Saa yaja sasa hivi,
    nitakapolinyakua kanisa langu.
    Mara tu baada ya tukio hili, Majanga, misiba,
    na mateso ya kutisha ambayo
    haijawahi kuwa humu duniani itaangamiza maisha mengi.
    Wakati adui yangu atachukua hatamu,
    hapatkuwa na
    toba tena,wala wakati wa kunitafuta ,kwani
    Mimi sitayajibu maombi yoyote,
    neema itakuwa imeondolewa na Roho wangu Mtakatifu
    hatakuwa ulimwenguni. Adui atachukua
    hatamu nanyi
    mtasaga meno yenu na kupiga mayowe
    mioyoni mwenu kwa mateso na kuvunjika.
    Zivunjeni nyoyo zenu sasa na mzifanye zimwage damu
    ya toba,zipasuenii nyoyo zenu kwa
    toba katika
    sekunde za mwisho za wakati uliosalia, la
    sivyo ghadhabu ya kutisha iwapate.
    Lakini watu hawa wana roho ya kuasi, nao wameasi na kwenda zao. Hakuna
    asemaye moyoni
    mwake, wacheni sasa tumuogope Bwana
    Mungu wetu apeanaye mvua ya sasa na
    hata ya awali
    katika wakati wake.Ametuhifadhi kwa ajili ya wakati teule wa mavuno. Uovu
    wenu umeyageuza
    mambo haya, na dhambi zenu zimezuia
    mambo mazuri kuja kwenu.
    Kwani miongoni mwa watu wangu
    panapatikana watu waovu, wananyemelea kama
    afanyavyo
    yule amtegae nyoka,wameweka mitego na
    wamewanasa watu. Kama vile kizimba
    kilivyojaa
    ndege basi ndivyo nyumba zao zimejaa udanganyifu, kwa hivyo wao wamekuwa
    wakubwa na
    tajiri sana.
    Wao wamekuwa wanono, wanang'ara, naam,
    wamezidi matendo ya waovu, wao
    hawahukumu vyema mambo ya wakiwa lakini bado
    wanafanikiwa; na haki za wanyonge
    hawazihukumu au
    kuzitilia maanani. (Jeremiah 5:24-28)
    Nyinyi hamtanyakuliwa asema Bwana,
    isopkuwa mbadilishe mienendo yenu na kutubu.
    Mimi sitawanyakua wale waliooana na
    televisheni, sinema na burudani ambazo
    zimechukua
    muda wenu mwingi nanyi hamna wakati
    kwangu miye Mungu na neno langu. Mimi sitawanyakua wakristu waendao kanisani
    jumapili pekee ili kutuliza
    ghadhabu yangu juu
    ya maisha yao ,nao wanadhani kwamba Mimi
    Mungu sioni wala kuyafahamu yale
    wafanyao. Jumapili, wao huenda tu kanisani kujionyesha
    nguo zao nzuri na kupiga gumzo
    na marafiki wao.
    Nyumba yangu imekua mtandao wa kijamii .
    Mimi Yesu Kristo, Bwana wenu sitawanyakua
    wale wanaoutumia muda wao mwingi kuitazama
    televisheni au katika kuvisoma vitabu vya
    riwaya na mambo mengine.Kwa
    sababu wamezigeuza
    riwaya hizi pamoja na mafunzo ya kisayansi
    kuwa washauri wao, badala ya kuwa na Roho
    Mtakatifu kama rafiki wao wa kweli tena bora.
    Muumini yeyote aliyesahau kumtafuta Roho
    Wangu Mtakatifu na amezifanya
    televisheni na itikadi
    zingine za kipepo kuwa marafiki wake wa dhati badala ya neno Langu ata
    achwa nyuma
    kukumbana na mpinga Kristu na alama ya
    mnyama muovu.
    ------------------------------
    *Page 3* 3
    Mapepo yamefaulu kujiipenyeza ndani na
    katikati ya kanisa na kanisa leo
    limegeuzwa
    kuwa na tabia na itikadi za kipepo, badala ya
    kuwa na neno Langu na tabia zangu Mimi Bwana
    Yesu.
    Kanisa kama hili lita achwa nyuma.
    Wale waishio maisha yao wakiitangaza miili
    yao kwa kuvaa miundo ya nguo
    iliyo chafu na isiyokuwa ya heshima, wakiiweka wazi na
    kuionyesha matiti yao na kuifunua
    miili yao;huu bila
    shaka ni mfumo wa kidunia. Wakrsitu hawa
    wananiambia Mimi Mungu wao, Mungu
    , tayari nimekupa moyo wangu na hiyo imetosha.
    Kuhusu sehemu yangu ya nje, niache
    niitunze kwa
    kuvaa nipendavyo.
    Wacha ijulikane kweli kwamba tayari ni
    mekwisha waacha muishi na kuufurahia ulimwengu.
    Kwani hamfahamu kuwa Mimi ni Mungu aliye
    na wivu? Mimi nina wivi kwa ajili
    yenu lakini nyinyi
    mnanishiriki na ulimwengu, kamwe sitokubali
    hivyo. Muumini yeyote ambaye amenigeuza kitu cha
    kuchezea asemaye moyoni mwake;
    Mungu sio
    mbaya hadi hawezi elewa kwamba tunaishi
    katika karne ya ishirini na moja na
    kwamba sisi huishi jinsi tuishivyo.
    Wakati wa Nuhu uovu ulikuwa mchache kuliko
    sasa, wakati wa luti hapakuwa na
    uovu kama leo,
    kwa hiyo tubuni la sivyo hamtakuwa na
    udhuru. Mimi sitawachukua wale wanunuao,kuuza na
    kucheza michezo siku yangu
    takatifu ya kuabudu ya
    jumapili au jumamosi.
    Siku yoyote ile viongozi wenu wameweka kwa
    ajili ya kuniabudu Mimi ni sharti iwe Yangu pekee,
    Mimi ndiye Bwana.
    Siku hii lazima itakaswe kwangu pekee. Watu
    hawaniheshimu Mimi Bwana na
    Mungu wao.
    Wao huniambia na kubishana na watumishi wangu wa kweli wakisema hii ni
    sheria nasi tu katika
    wakati wa neema.Kwani Bwana wenu hawezi
    kuheshimiwa na kuogopwa?
    Kwani neema yamaanisha kumkosea heshima
    Mungu wenu? Nyinyi hubishana nami hata
    maombini namna vile mtabishana muunapo
    ujumbe huu.
    Mimi sitawachukua waongo,wenye kiburi,
    waumini wabatili ambao marafiki wao
    wakuu ni watu wa kawaida nao hujipotosha wenyewe na
    ulimwengu. Mimi Bwana na Mungu wenu
    nimewaamuru
    katika neno langu jitengeni kutoka miongoni
    mwao nanyi msijihusishe na
    kongwa zisizo sawa. Mimi sitawachukua wale waongezao maneno
    yao ndani ya ukweli , wale
    wawasengenyao
    watumishi wangu na wachungaji ambao
    hunitumikia kwa kweli na kulibeba neno
    langu. Ole wake Yule aongezae na kuondoa kutoka kwa neno
    langu la unabii !
    Huu ndio msimamo wangu, kubalini au kataeni
    asema Bwana.
    Mimi Yesu mesia, Mungu wenu na hapana
    mwingine. Jitayarishe ,jitayarishe Mimi naja upesi!

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate