Wafilipi 2:10-11
  • KITABU: UBATIZO WA KWELI KWA ULIMWENGU WOTE (KITABU CHA NABII HEBRON)


    KITABU: UBATIZO WA KWELI KWA ULIMWENGU WOTE

    Kitabu kimeandikwa na Mtume na Nabii Hebron Wilson Kisamo

     

    UBATIZO WA  KWELI KWA ULIMWENGUWOTE


    YALIYOMO

    1.      UBATIZO NI NINI ?

    2.      UBATIZO WA KWELI

    3.      FAIDA ZA UBATIZO WA KWELI

     4.      HASARA ZA KUBATIZA KINYUME NA MPANGO  

              WA  MUNGU.

        

    5.     JINSI MUNGU ANAVYOTAKA UBATIZO  

             UFUATWE

    6.       SALA YA TOBA


           TOLEO LA KWANZA

            9.8. 2012

            ISBN 978-9987-9553-2-9





    UTANGULIZI

     Ndugu nakusalimu kwa jina la YESU  KRISTO, ambaye ndiye Bwana na Mwokozi  wa Mataifa yote, pia ndiye Mfalme wa wafalme na BWANA  wa mabwana na hapana Mfalme mwingine zaidi yake. Mimi jina langu naitwa Hebron Wilson Kisamo, YESU amenichagua nimtumikie yeye kwa jinsi anavyotaka yeye ili kukomboa ulimwengu huu ambao umepotea  na shetani ameumiliki kwa asilimia 98% sawa sawa na  YESU alivyoniambia mwenyewe. Amenituma ulimwengu wote ikiwa inamaana nchi zote, mabara yote. Ujumbe huu aliniagiza  rasmi na kunipa  mamlaka yake  tarehe 14.06.2010. Na akanipa jina la Kanisa lake niliite  YESU NI BWANA NA MWOKOZI  WA MATAIFA YOTE INTERNATIONAL MINISTRY.  Akaniambia  mwanangu nitautumia huu mwili wako kuukomboa ulimwengu wote, utachukiwa sana,utafanyiwa na kuitwa majina mabaya lakini usiogope tena ufurahi zaidi, kwani mimi  YESU walinifanyia mabaya  zaidi na ya uongo  yakitokea kwa baba yao wa uongo ambae ni lusifa, nilifurahi daima.

    Hakuna jambo lolote litakalofanikiwa juu yako au silaha yoyote juu yako, nipo na wewe milele. Nitakutumia kwa namna ya tofauti na kwa kiwango kikubwa sana ambacho hakijaonekana tokea kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu huu. Adui yako ni adui yangu, akasema YESU kwa sauti ya uchungu sana, watumishi wamenisaliti maagizo niliyowapa hawayafanyi na wamegeuza  NENO langu kuwa maandiko badala ya Neno, maandiko yanatoka kwa shetani maana lusifa anaijua Biblia yote, na maandiko hayana uthibitisho wa nguvu zake YESU. Neno  linatoka kwa YESU na lina udhihirisho wa nguvu za  MUNGU. Napia wana wa adamu wanateseka wanalia na kuomba hawapati majibu, na zaidi wanazidi kupotoshwa na viongozi wa kanisa, maagizo niliyoyaacha nilivyokuwa ulimwenguni kabla ya kurudi kwa BABA yangu ili kuniandalia maandalizi ya ujio wangu ili nipate kuwaponya wengi waende mbinguni, imekuwa kinyume idadi kubwa ni ya watu wa shetani. Waliokuwa  watumishi wangu wamenisaliti 98% sipo nao. Wameamua kwenda kuzimu, na shetani anawatumia na jinsi anavyowatumia, ni kubadili au kwenda kinyume na agizo la MUNGU, mfano watumishi kwa sasa wamefanya kanisa ni mahali pa biashara, kunyanganya  watu vitu vyao na wakijua  wamenitolea mimi, na kunifanya mimi YESU  ndiye mnyanganyi, kwa midomo yao hunitaja kama wananipenda ila mioyoni mwao hawapo na mimi, wamekuwa watumishi wa pesa na sio mimi, wamekuwa wakitenda miujiza lakini siyo yangu ni miujiza ya shetani, na hao ni kati ya wale ambao siku ya mwisho nitawakataa na kuwaambia sikujui. Kanisa  limeniacha kunitegemea mimi, imebaki 2 % tu ulimwengu mwote. Sasa  mimi YESU ninalikomboa kanisa mwenyewe na ndipo unabii na utukufu wa kanisa la mwisho utakuwa mkubwa kuliko wa kanisa la kwanza unatimia sasa.



    SHUKURANI

    Namshukuru  Mke wangu sana kwa kunitia moyo na kuniombea, nawashukuru watumishi wote wanaoniombea na kutumiwa na MUNGU kutumika pamoja na YESU aliyeniita, mkono wa MUNGU uwe juu yao siku zote za maisha yao. Asante.

    MTUME NA NABII – HEBRON WILSON KISAMO

    KIONGOZI NA MWANZILISHI  WA HUDUMA

    KANISA LA YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE

    INTERNATIONAL MINISTRY.

    P. O. BOX 13657

    ARUSHA, TANZANIA

    EAST AFRICA

    EMAIL: publications@prophethebron.org



    1.     UBATIZO NI NINI?

    Ubatizo ni kiapo kati ya mwanadamu na MUNGU  aliye hai, Aliye uumba ulimwengu  pamoja  na wewe ndugu msomaji wa kitabu hiki; Ubatizo ni agano lako wewe na MUNGU ya kwamba wewe ni wake  wala sio wa mwanadamu au kitu chochote.

    Ubatizo chanzo chake ni MUNGU mwenyewe  ndiye aliyepanga akiwa anayo maana nzuri na njema sana kwa ajili  ya mwanadamu ambaye ni yeye mwenyewe aliyemuumba  kwa faida yake yeye mwenyewe MUNGU, moja wapo ya sababu amemuumba ili amuabudu yeye tu , na sio kitu  kingine  chochote, sababu nyingine  akatawale kila kitu maana hivi viumbe vyote  aliviumba ili  mwanadamu avitawale ( Mwanzo 1:26 ). Baada ya anguko la mwanadamu  shetani akauvuruga ulimwengu  akijua kwamba ndiyo ameshinda na atatawala ulimwengu  na  wanadamu wote, baada ya haya kutokea. Ndipo MUNGU  akaanzisha huduma ya ubatizo, ili kuwasafisha  na kuwakomboa  wana wa Adamu kupitia maji, kwanza kabisa MUNGU alimtuma Yohana aje ulimwenguni  kuja kubatiza,  Yohana ni mnaziri wa MUNGU  aliyetoka mbinguni kama YESU alivyotoka mbinguni, akiwa  Mbinguni  alitumwa  na Baba kuja kutengeneza njia  yani YESU.  Yohana 1 : 15 -18 ) . Na kabla ya ujio wa Yohana , nabii  alitabiri  juu ya Yohana  na nabii Isaya alitabiri pia, na ikatokea.  Yohana akazaliwa na Elizabeth na YESU  ilitabiriwa hivyo hivyo na ikatokea, hawa wote ukiangalia hata jinsi wazazi wao walivyopata ujauzito ni kwa njia ya Roho Mtakatifu. ( Mathayo 1 : 18 – 24 ) , ( Luka 1: 11 – 38 )  Au kwa njia ya mpango wake MUNGU  mwenyewe, ili kuukomboa ulimwengu  huu, Yohana akazaliwa na akayatenda yale yote aliyoagizwa na MUNGU aje ayafanye ulimwenguni  humu. Aliyafanya na alibatiza sawa sawa  na alivyoelekezwa na MUNGU.    (Mathayo 3 : 11 – 12 ) . Yohana alibatiza  kwa maji ikiwa na maana kuwasafisha.

    Ndugu msomaji wa kitabu hiki, natumaini mpaka sasa umeelewa ubatizo ni nini? Na chanzo chake  ya kuwa ni MUNGU mwenyewe ndiye muanzilishi. Na wakati  Yohana akibatiza mara nyingi alikuwa akielezea habari za YESU na pia kusema ya kuwa yeye ni mkuu sana hata yeye Yohana alikiri  kabisa hastaili hata kuvichukua viatu vyake; Ndugu msomaji hapa hata Yohana alietoka mbinguni akatumwa ulimwenguni anakiri YESU ni Mfalme na  yeye atabatiza kwa Roho na kwa moto ( Mathayo 3 :11 ).  Na hata Yohana aliogopa  kumbatiza YESU  kwa ajili ya ukuu alionao lakini  YESU  akamwambia Yohana , Kubali hivi sasa ; kwa kuwa  ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote, basi akakubali , na YESU alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini, na tazama mbingu zikamfunukia akamwona Roho  wa MUNGU akishuka kama hua, akija juu yake, na tazama sauti kutoka mbinguni ikasema, “ Huyu ndiye mwanangu mpendwa wangu ninayependezwa naye.  ( Mathayo 3: 15 -17) . Ndugu msomaji na mtoto wa MUNGU  tena umefanana na yeye MUNGU  azidi kukufungua ufahamu wako zaidi ili uelewe zaidi kuhusu ubatizo aliouagiza MUNGU watu wote wabatizwe.  Ukisoma katika injili ya ubatizo wa Yohana utaona ameyafanya yote aliyoagizwa na MUNGU ili tu wewe ukombolewe  maana pasipo wewe kubatizwa  huendi mbinguni ( Yohana 3 : 5-7 ) .

    YESU alibatizwa kwa maji mengi na alibatizwa kwa maji mengi  kwa maana ndivyo alivyoagizwa na akafanya kama  kama yeye alivyotakiwa afanye na MUNGU, na YESU alikuja ulimwenguni ili kutukomboa na kwa sababu alikuja ulimwenguni kwa njia ya mwili ilimbidi na  yeye abatizwe na kupitia ubatizo aliobatizwa na  sisi sote tubatizwe  kama yeye ambaye ndiye tunaemwamini na ndie njia ya uzima na ukweli. ( Yohana 14 : 6 ).

    Na MUNGU alipo mtuma  Yohana  kubatiza, hakumwambia mtu akibatizwa awe na msimamizi mwanadamu, msimamizi wa ubatizo ni Roho  Mtakatifu.

    Utaona baada  na hata kabla ya YESU kubatizwa hakuwa na mwanadamu msaidizi / msimamizi. Sasa mpaka hapa natumaini  unazidi kuelewa kuwa katika ubatizo msimamizi ni Roho  Mtakatifu na siyo mwanadamu,angalia mfano alivyobatiza Yohana na mpaka  YESU alivyobatizwa na pia wale mitume wa YESU jinsi walivyobatiza, nao waliwabatiza watu bila wasimamizi wanadamu. Watu waliobatizwa walisimamiwa na Roho Mtakatifu tu, na ndio mpango wa  MUNGU, mdhamini wa ubatizo ni Roho  Mtakatifu. Lakini  siku hizi  agizo aliloagiza MUNGU limeachwa, siku hizi mdhamini wa ubatizo ni mwanadamu tena lazima awepo mwanamke na mwanaume. Huu sio mpango wa YESU ni mpango wa shetani ili kuangamiza watu wasiende mbinguni. Siri hii kaniambia YESU, waambie ulimwengu mzima hashiriki ubatizo huo ni feki. Baada ya ubatizo Roho Mtakatifu alimshukia  YESU ili kumshuhudia ya kuwa ni mwana wa MUNGU na baada  ya kushukiwa na Roho Mtakatifu, hapo ndipo   YESU akaanza kuongozwa na huyo  mdhamini ambaye  awaushirika na MUNGU ( 100% )  akamwongoza kuyashuhudia matendo ya MUNGU, kumtia nguvu, mwana wa MUNGU.  Hivi ndivyo inavyotakiwa katika ubatizo ni Roho Mtakatifu tu, siyo mtu asimamie mtu. Hayo ni mapokeo ya mwanadamu, ambapo baada ya YESU kupaa kwenda mbinguni shetani akawaingia wale ambao hawakumtii Roho Mtakatifu kubadili mpango wa MUNGU katika ubatizo. Na walibadili hata ubatizo wa maji mengi baadhi yao wakaanza kubatiza kwa kutumia beseni au kikombe tena ni vitone vya maji kichwani tu !  Nikuulize  wewe je Yohana ndivyo alivyobatiza ? Jibu ni Hapana.

    Na kama jibu ni hapana , hata kwa MUNGU ni hapana , na hata mbinguni ubatizo huo haupo na kama haupo mbinguni umetoka wapi ? Jibu ni kwa shetani, haijalishi jina la YESU linatajwa hata Roho Mtakatifu kutajwa , huo ni ubatizo feki. Ameniambia YESU niueleze ulimwengu wote ikiwa inamaana  mataifa yote, watu wote wa rangi zote na kabila zote bila mipaka watu wajue ukweli wake na wamjue  YESU wa ukweli, maana jina lake  linatumiwa vibaya  na watoto wake  wanaangamia,  kwa ajili ya watu walioubadilisha mpango wake  MUNGU. Akasema  mwanangu Hebron  watoto wangu wananipenda sana ila hawambiwi ukweli kuhusu mimi 98%  shetani ameuteka ulimwengu wote imebaki 2 % tu ndio wananijua kiukweli, sasa waeleze wabatizwe  ubatizo niliobatizwa mimi YESU,  watu wanajua kwamba mimi ndimi njia ya uzima na ukweli na hakuna atakayefika kwa Baba  pasipo mimi YESU, na mimi YESU nilikuja ulimwenguni kuionyesha njia ya kwenda  kwa Baba yangu, Baba yangu hakuwa mjinga kuagiza ubatizo wa maji mengi, hakuwa mjinga kumwambia Yohana  mtu akibatizwa  awepo na msimamizi. Leo hii  nafasi ya Roho mtakatifu  imechukuliwa na wanadamu, matokeo yake ni ubatizo  batili, nakuuliza wewe unayempenda YESU je? YESU alivyobatizwa alikuwa na wadhamini? Jibu hapana. Hivyo ndivyo inavyotakiwa, mdhamini wako  ni Roho mtakatifu na ndie atakae kuongoza na kukuombea  maishani  mwako na kukupeleka mbinguni.

    Nakuuliza swali ili uzidi kufunguka ufahamu wako. Je ! mwanadamu ndie atakayekuongoza wewe ufike mbinguni ? Jibu ni hapana, ( Roho Mtakatifu ndiye atakaye kuongoza ufike mbinguni na kukushindia hapa ulimwenguni kama alivyo mshindia YESU ).

    MUNGU hakuwa mjinga kutupa Roho Mtakatifu awe mdhamini  katika ubatizo wake yeye, alijua kwamba, Roho Mtakatifu ana umoja na yeye au kwa lugha  rahisi ili wewe uelewe, Roho Mtakatifu ni moja wapo ya nafsi ya MUNGU, Tunajua kwamba zote zina umoja ( MUNGU Baba, Mwana , na Roho mtakatifu ) na lile kusudi la kiapo cha ubatizo  walipanga wote  hawa watatu  ili kukupata wewe, sasa  nakuulizwa  swali kama wewe haujadhaminiwa na Roho Mtakatifu utaenda wapi ?  Jibu ni  jehanamu. Badilika ubatizwe  ubatizo kama YESU  alivyobatizwa,  Yeye ndio kweli na njia yake ifuatwe hakika  utapona ( Yohana  4:6)  usifuate mapokeo ya dini  fuata mwongozo wa ubatizo ulioandikwa kwenye Biblia au kitabu kitakatifu cha MUNGU.

    Safari yetu ya mbinguni  na maelekezo yote yameandikwa ndani ya kitabu hiki  na katika kitabu cha ufunuo wa Yohana  22 :18 – 19  MUNGU ameonya  ole wake atakayeongeza au kupunguza ya nabii wa kitabu hiki, sehemu yake itaondolewa  katika ule mji mtakatifu. Sasa ndugu msomaji embu chunguza kwenye Biblia kuanzia kitabu cha kwanza  mpaka cha mwisho, hakika  ( 100 %)

    Hautakuta ubatizo wa maji ya kikombe  yaani kichwa tuu ndio kiwekwe maji, hamna mdhamini mwanadamu  katika ubatizo, sasa hapa utaona kabisa ubatizo umeongezewa mambo nje ya MUNGU alivyopanga na huu ni mpango wa shetani ili wewe usiende  mbinguni. Maana tayari umeenda tofauti na y eye MUNGU. Ni kuulize swali je MUNGU ni mjinga aliposema mtu abatizwe kwenye kijito cha utakaso na azamishwe  mwili wote? Jibu ni hapana.

    Na je embu fikiria na ufunguke ufahamu wako uwe huru je! Kwa nini ni kichwa tu kinamwagiwa maji tena matone tu !  Je mpango wa MUNGU  wa kuzama kwenye maji kama Yohana alivyobatiza umetimia ? na je  huo mwili umeingia kwenye maji wote? Jibu ni kichwa tu kimemwagiwa maji na  viungo vingine hamna kitu,  sasa ujumbe huu amenieleza  YESU na akanifundisha, kweli niliogopa sana baada ya kuujua ukweli halisi, akaniambia nilisha sema sana  na baadhi ya watumishi wangu waseme kweli kwa mataifa yote, wamenisaliti,  wananitaja tu jina langu  midomoni mwao baadhi yao ni wanafiki, lakini ole wao mwisho wao umefika ni wakati wangu sasa mimi  YESU nahitaji mwili wako tu  kama nilivyoutumia  mwili wa Paulo lazima watu wanirudie mimi na  kazi hii  ameianza  YESU mwenyewe  tokea  (April 2012 ), Dunia nzima, na njia za kuzimu  zote alinipa  maelekezo ya namna ya kuzifunga kwa hiyo waliokuwa wanategemea kuchukua nguvu sasa hawana pa kuzipata  wataporomoka mpaka (zero) haswa watumishi wanaotumia nguvu za giza. Hii ni kwa ulimwengu mzima na tayari wanajua  mambo hayaendi.


    2.     BATIZO WA KWELI

    Ubatizo wa kweli  ni ubatizo aliouagiza MUNGU, uwe ni ubatizo aliobatiza Yohana  na ubatizo aliobatizwa  YESU tu. Huo ndio ubatizo ambao upo hata kwenye mafaili ya MUNGU  na ndio anaoutaka.  Na kama ubatizo uliopo mbinguni ni huu, basi ndio ufuatwe . Maana ndiyo anaoutaka na aliuandaa kwa  ajili yako wewe ili upone, sasa kama umeukataa ubatizo alioutaka MUNGU na ukabatizwa  ubatizo asio utaka yeye, haijalishi jina lake linatajwa huo ni ubatizo batili haumuhusu yeye, hayo ni mapokeo kutoka kwa waanzilishi  walio mkufuru Roho mtakatifu , na wapo kuzimu.

    Nilionyeshwa na YESU, tena dini zao ni kubwa kwa majina sana ulimwenguni.

    Wamefungwa minyororo na YESU akaniambia hawa wanasubiri moto siku ya mwisho. Wamemkufuru Roho Mtakatifu, na wanateseka sana, walikataa kumtii MUNGU na  wakamkufuru Roho mtakatifu, sasa  wanakushangaa wewe unaengangania dini, unasema  nitakufa na dini ya wazazi wangu ! Dini salama ni YESU tuu, ndio umtegemee yeye tu utapona.

    Ubatizo wa kweli lazima taratibu zote  alizofuata muasisi wa kanisa  yaani YESU, ndizo zifuatwe ikiwa ina maana alichokifanya YESU ndiyo salama na ndiyo kweli na alifanya ili sisi tufuate njia aliyotuonyesha.

    Mtoto mdogo abarikiwe tu kwa kuwekwa  wakfu kama YESU alivyowekwa wakfu na  kubarikiwa akiwa mototo,  MUNGU  aliandaa na kumpa ujumbe mtumishi wake Simon soma ( Luka 2 :29 ).  YESU alipobarikiwa alikuwa mototo tena hajijui  na alipokuwa mtu mzima  au anao ufahamu ndio alibatizwa. Huu ndio mpango wa kweli na uliopo  mbinguni na hata Yohana alitimiza na YESU akafanyiwa hivyo hivyo. Na kama unataka  kuwa mfuasi wa YESU lazima ufuate taratibu zake  hapo utakuwa kama yeye na utapokelewa na Baba yetu wa mbinguni, awafurahia na wazee 24 na malaika wake na serekali yake inafurahia.

    Huo ubatizo mwingine hawafurahi kabisa, na ameniambia waambie wanangu wanielewe nawapenda.


    3.     FAIDA ZA UBATIZO WA KWELI

    Unaanza  kubarikiwa tokea ukiwa mototo mdogo kama YESU alivyobarikiwa akiwa mtoto. Na mtoto anakuwa mikononi mwa MUNGU, na MUNGU anaanza kumtengeneza kiroho na kimwili.  Na mtoto atakuwa mwema na anatabia njema, na ndani yake anayo hofu ya MUNGU.

    Unashiriki ubatizo alioutaka MUNGU Baba muumba wa vitu vyote ikiwamo na wewe, na unashiriki kiapo kamili kama YESU.  Na zaidi utajazwa nguvu za Roho Mtakatifu kama YESU alivyoshukiwa na  Roho mtakatifu ndiye anakuwa kiongozi wako milele na atakupeleka  mahali alipo MUNGU kama YESU alivyopelekwa tena,  kwa kushiriki hatua alizozitaka yeye mbingu inakuwa wazi. ( Yohana 3: 5- 7 ).



    4.     HASARA ZA KUBATIZWA KINYUME NA MPANGO WA MUNGU.

    A.      Hasara moja wapo wewe unakuwa umeshiriki jambo ambalo 

                        halipo hata mbinguni na hata kwenye kitabu cha muongozo wa   

                        kwenda mbinguni ( Biblia ) . Jambo  lingine unakuwa umeshiriki    

                        kuvunja amri ya MUNGU, ( Kumbukumbu la torati 5. 8 -9 ), 6: 14 - 

                        16). Na pia unabeba  laana maana unamjaribu MUNGU. Unatumia  

                        jina lake na unafanya kinyume na yeye alivyotaka,na ukifanya  

                        kinyume na yeye  tayari unaabudu miungu mingine.

    B.     Mtoto anakuwa katika msingi usio wa MUNGU wa kweli,  haijalishi jina la YESU  limetumika. Mtu huyo ataishi kwa kushikiliwa na shetani na ndiyo maana unakuta mtoto hadi kufikia mtu mzima unajuta kwa nini umemzaa, anavuta bangi, anakuwa mwizi, mtukutu, ni mtu wa ajabu. Hii ni sababu ya kwenda kinyume . YESU alipelekwa kwenda kubarikiwa akiwa mtoto, sasa siku hizi mtoto anabatizwa kwanza,  halafu akiwa mtu mzima ndio anabarikiwa ! Je, huu ndio mpango wa MUNGU?

    Jibu ni hapana. Mtoto angewekwa wakfu kama YESU , haya mabaya yote yasingempata, angeanza na baraka, ndio msingi wake MUNGU. Hiyo ndio sababu moja wapo na shetani awashitaki kwa MUNGU. “ Si unaona hawafuati ’’ Japo  yeye mwenyewe shetani anakutengenezea kosa ili uangamie na hapo hapo anakushitaki tena, ona jinsi shetani alivyomnafiki na ni mbaya sana.

    C.     Hasara nyingine huendi mbinguni unakuwa umeshiriki kiapo ambacho siyo kiapo amekitaka yeye MUNGU ili ukombolewe. Na MUNGU hakubali kiapo ambacho hakijatoka kwake! Nikuulize je wewe utakubali kusaini mkataba ambao haukuhusu?  Jibu ni hapana, hutasaini. Hivyo ndivyo ilivyo kwa MUNGU.

    D.     Hasara nyingine ni ule wakati wa wewe kubatizwa ndio unapelekwa kubarikiwa ukiwa mtu mzima. Hasara unayoipata hapa majira yako ya baraka na ubatizo wa MUNGU kwako yanakuwa yamepitwa na wakati na MUNGU huenda na wakati, ndio maana kuna majira ya kupanda na majira ya kuvuna, kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka. Kwa hiyo haupati kitu kutoka kwake.

    E.     Wewe unakuwa  ni wa dini na sheria tu.

    F.     Hautaki wokovu unakuwa mgumu maana  nafsi yako imeshikiliwa na mapokeo ambayo hayajatoka kwa MUNGU na kama hayajatoka kwa MUNGU na kama hayajatoka kwa MUNGU ni ya mpinga kristo. Haiwezekani wewe  ni mkristo  halafu unapinga wokovu, ( Warumi 10: 9 -11) ina maana  ndani yako ipo roho ya mapokeo ya dini  na mapokeo  ya mwanadamu, hawajui yametoka wapi, ni ya shetani na ile roho haimtaki YESU aingie ndani yako. Huu ni upofu ambao shetani ametumia njia mojawapo kuliteka kanisa na wewe unaekataa wokovu sasa, ufunguke uokoke.  Kupitia ubatizo feki alioniambia YESU, mtu anakula kiapo na dini yaani yeye ni wa dini tu na siyo wangu na ndio maana mtu huyo hanitaki kabisa. Mtu huyo hatanikubali tu mpaka   ile roho ya dini na mapokeo itoke ndani yake. Maana ndani yake ni roho ya kuasi inamshikilia. Na roho ya kuasi ikiwa ndani yake  haijalishi ni kwa mtumishi au muumini, atashiriki pombe, tena hata atazibariki , atafanya uchawi, kuoa wake zaidi ya mmoja bila hofu ya MUNGU na hata ubarikio na batizo zao watashiriki vitu vya shetani.

    Sasa nakuuliza ,  je ! YESU anashiriki hayo, au Roho mtakatifu anaruhusu disco kwenye sherehe  za ubarikio au ubatizo? Jibu ni hapana. Kwenye hizo sherehe mapepo na roho mchafu ndio huja kushiriki na kufurahia ya kwamba mpango waliopanga wa kukuangamiza umetimia.  Wacha sherehe za pombe, disco na mila.



    5.     JINSI MUNGU ANAVYOTAKA UBATIZO UFUATWE

    a.      Mtoto mdogo akizaliwa apelekwe madhabahuni awekwe wakfu tena iwe madhabahu ya kweli iliyo hai ambayo YESU anakaa hapo.

    b.     Mtu akiwa na ufahamu aokoke kwanza kwa hiari yake mwenyewe  ndio abatizwe kwenye maji mengi tena yanayotembea. ( kijito cha utakaso) siyo kisimani.

    c.      Mwili wote uzamishwe kwenye maji kama YESU alivyobatizwa.

    d.     Angalia anaekubatiza awe kweli ana roho wa MUNGU ndani yake, maana kama ni roho wa shetani yupo ndani yake hawezi kukushirikisha ubatizo mtakatifu wa MUNGU, ( Hapo ubatizo ni feki ).

    e.      Ubatizwe kwa jina la Baba , Mwana na Roho Mtakatifu .

    f.        Usikubali kubatizwa kwa jina la mtu au kitu chochote tofauti na YESU

    g.     Usikubali kubatizwa na nabii wa uongo, hapo anakuwekea  maraho yake na shetani aliye ndani yake ili akunajisi usiende mbinguni.

    h.     Usitoe pesa za malipo ndio ubatizo, YESU hakutoa na wewe fanya hivyo hivyo.


    6. SALA YA TOBA

    Kwa wewe  ambaye  hujaokoka na unapenda kuokoka.

    UTASEMA MANENO HAYA:

    Bwana  YESU,  nipo mbele zako naomba  Rehema, unisamehe makosa yangu naomba uandike jina langu kwenye kitabu chako cha uzima  wa milele; Bwana YESU nishike mkono, mimi ni wako kuanzia sasa .  AMEN !

    MUNGU akubariki sana  akutunze,  milele na Roho mtakatifu akuongoze mahali alipo YESU wa kweli ndio akupeleke hapo ukasali hapo. AMEN.



    NOTE:

    Ujumbe huu  ameniambia YESU ni kwa watu wote wa ulimwengu huu. Na mtu yeyote ambaye amebatizwa kinyume na MUNGU alivyoagiza, waambie hawajabatizwa na mimi YESU sihusiki kabisa, maana  ubatizo huo haujatoka kwa Baba yangu  ni ubatizo wa mapokeo , haijalishi walitumia jina langu kama pazia hivyo hukumu  inawasubiri. Injili yangu imebadilishwa,na ndio maana watoto wangu hawanioni, wamefungwa  na shetani, na yeyote anae fanya kazi yangu kinyume  na nilivyoagiza, tayari amekuwa nabii wa uongo, mtu yeyote akiongeza neno langu au kupunguza huyo ni mwongo, sina furaha naye hata Baba  yangu na malaika wa mbinguni wote. Ole wao mwisho  wao  umeshafika.  Narudi kuchukua ulimwengu na kuwakomboa wanangu mwenyewe.  Na Tanzania ndio Edeni,  mimi MUNGU nimeichagua , na Mataifa yote yataponea hapa na kunijua mimi YESU .

    Haya ni maneno aliyo niambia YESU na nimeyanukuu kama alivyoniambia.


    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate