Wafilipi 2:10-11
  • JIANDAE KUKUTANA NA MUNGU WAKO! FALME ZA MBINGUNI NA KUZIMU,NA KURUDI KWA KRISTO NA Angelica Zambrano USHUHUDA WA PILI

    www.DivineRevelations.info/2v Imefasiriwa na Peter Kahale Katika safari yake ya pili, Angelica
    alionyeshwa hukumu dhidi ya Wakristo
    wanaomuibia Mungu katika zaka
    na sadaka, hukumu dhidi ya watawa
    wanaofanya ibada ya sanamu na watoto
    walioasi, kitabu cha uzima cha Mwanakondoo, na mengine zaidi. "Waambie watu wangu kwamba kuja
    kwangu ku karibu, Nitakuja kwa watu
    wangu watakatifu, waambie watu wangu
    kwamba ni watakatifu tu ndio
    watakaoniona mimi." Januari 4, 2010, 05:50 usiku, Empalme,
    Ecuador. Bwana alimchukua Angelica
    kwa mara ya 2.
    Nakala hii imechukuliwa kutoka katika
    video ya ushuhuda ya kihispania. Angelica: Saa 6:00 usiku wa manane, baadhi ya ndugu kutoka kanisani
    walifika katika nyumba yangu, basi
    vyombo vya habari viliwasili, na kila
    kitu kilichukuliwa katika kumbukumbu.
    Nilikuwa juu ya kitanda, ghafla, nikaona
    malaika wawili. Kama vile ilivyokuwa mwanzo, walinichukua
    mikono yangu na kusema, "Inuka, kwa sababu Mfalme wa wafalme
    na Bwana wa mabwana
    anakusubiri." Nilipoinuka, niliona mwili wangu umelala hapo, na watu wengine waliokuwa katika chumba
    hicho. Nilianza kutembea. Nilinyoosha mikono yangu kwa malaika
    na tulianza kuelekea juu. Tulikuwa tunakwenda haraka sana, na
    katika sekunde chache tulifika mbele ya Bwana. Nikasikia
    Malaika wakiabudu, "Haleluya ... Mtakatifu, Mtakatifu."
    Nilikuwa na furaha. Katika Ufalme wa Mungu kulikuwa na
    bustani nzuri sana. Niliona Bwana
    akinikaribia. Akasema, "Binti, nimekuwa nikisubiri, kwa sababu
    nina mambo mengi ya kukuambia", "Bwana, mimi hapa, nataka kukaa na Page 2 2 wewe. Sitaki kurudi Duniani, tafadhali
    napenda kukaa na wewe. "Bwana
    akajibu, "Mtoto wangu, una mambo mengi ya kufanya. Una kazi, imekupasa
    ufanye kazi yangu. Nitakuonyesha kitu
    kwa ajili ya maisha yako, kitu kwa ajili ya watu wangu, na kitu maalum
    kwa ajili ya watu, kwa sababu nataka
    uokoe binadamu na sitaki mtu yeyote apotee. " Kisha, niliona malaika wawili, Mikaeli na
    Gabrieli wamebeba vitabu vikubwa; vitabu hivi
    vilikuwa vizuri sana na vinang `aa.Nilipokuwa
    nikiangalia vitabu hivyo, niliuliza, "Ni nini hii?" na Yesu akasema, "Je, unataka kujua ni nini kilicho katika vitabu
    hivi?" Nikajibu, "Ndiyo Bwana." Akasema, "Mikaeli, fungua." Malaika Mikaeli alipoanza kufungua kitabu,
    niliweza kuona maandishi ya dhahabu,
    kama namba, lakini sikuweza kuelewa. Niliwaza, "hiki ni nini?", Na
    Malaika Mikaeli akajibu, "Maandishi yote haya na namba unazoona zimeandikwa hapa ni wale watu
    duniani ambao wamemkubali Bwana
    wetu kama Mwokozi wao wa pekee, kwa mafunuo yale ambayo
    alikufunulia ulipokuwa pamoja naye . "Nilipatwa na msisimko na nikamuuliza, "Ni watu wangapi wamo humo?" Alinipa
    jumla ya idadi ya roho katika maelfu. Moyo ulivunjika na nikaanza kulia,
    nikisema, "Bwana hizo ni roho/nafsi
    nyingi ambazo ni waongofu", Akaitikia, "Unaweza kuona, malaika huyu, Malaika Gabrieli ana jumla ya
    idadi ya watu wale ambao walikuwa wamejitenga mbali na njia
    zangu na kuwa sasa wamekuja
    kwangu, wamekuja kwangu mwanangu. "Nilitazama katika idadi ile na niliona ni kiasi kikubwa. Nikasema,
    "Bwana hii ina maana taji yangu imejaa lulu na kwamba sasa
    utaniacha hapa katika Ufalme wako?"
    Bwana alijibu, "Hapana mwanangu , muda wako wa kuja
    hapa bado, imekupasa urudi Duniani.
    Je, ungependa kuona taji yako?" Nilijibu kwa msisimko, "Ndiyo Bwana,
    ningependa kuona taji yangu," Alisema, "Malaika Gabrieli,
    mletee taji yake." Niliona Gabrieli amebeba tray kubwa sana,
    yenye taji nzuri, lakini yenye lulu chache juu yake. Nilimuuliza,
    "Bwana, taji hii ni ya nani? Akanijibu," Hiyo ni taji yako mwanangu.
    "Nikamuuliza," Lakini Bwana, kwa nini taji yangu haijajaa lulu,
    kama nafsi/roho nyingi zimekuja kwako Bwana? "Naye
    akanijibu, "Binti, bado njia ndefu inakusubiri,ni roho/nafsi 3,500
    tu zimekuja mbele yangu, lakini
    imekupasa kwenda na kuhubiri neno langu kwa sababu kuna roho
    nyingi bado ambazo zinatakiwa kuja
    kwangu." Lakini Bwana, kwa nini nisibaki hapa tu? Yeye aliniambia, "Binti, kwa sababu taji ya uzima
    inapaswa kujaa lulu. Nikasema, "Sawa Bwana, Nitatekeleza kazi yako." Kisha
    akasema, "Nina jambo la kukuonyesha Mwanangu." Bwana alinichukua, na kwa haraka
    tulishuka kutoka mbinguni na kuingia
    ndani ya tundu/tanuru la kuzimu, kama ilivyokuwa mara ya kwanza wakati
    nafunuliwa kuhusu kuzimu. Nilisema,
    "Oh! Bwana, nini kinachotokea?" Yesu alisema, "Ninajambo la kukuonyesha kuzimu," "Lakini Bwana Sitaki kuwa hapa. Bwana, kumbuka uzoefu/ufunuo wetu
    wa kwanza, tayari ulinionyesha mambo
    mengi", Alisema, "Ndiyo mwanangu, lakini sasa mambo
    mbalimbali tofauti, nitakuonyesha. " Tulikwenda chini kati ya miali ya moto
    zaidi, na nikaanza kulia. Haikuwa rahisi
    kuwa pale. Nilisema, "Bwana, Page 3 3 nataka kutoka nje ya hapa, tafadhali
    nisaidie, nisaidie." Nilisikia mamilioni ya
    watu, baadhi ya watu walikuwa wakisema, "Oh Bwana, nihurumie, nisaidie tafadhali, Bwana, nipe nafasi nyingine." Miongoni mwa wale watu, nilisikia mtu
    mmoja akisema, "Ninaomba msamaha wako sasa Bwana, kwa
    sababu nimekuibia, nisamehe kwa
    kuiba, Nilikuibia Bwana na sitaki kufanya hivyo
    tena." Mimi niliuliza, "Bwana, ni nani na kwa nini yeye anasema
    alikuibia?" "Mwanangu nitakuonyesha yeye ni nani." Tuliingia kwenye selo yake na nikaona mtu aliyeharibiwa. Miali ya moto ikafunguka
    na nikamuona alikuwa akiungua. Watu wote walio kuzimu wana nembo/
    kibao juu ya vifua vyao, na 666 kwenye paji za nyuso zao. Mtu huyu
    aliunyosha mkono wake na kusema, "Bwana nisamehe." Mimi nilimuuliza, "Mbona uko hapa,na kwa nini unamuomba msamaha Bwana, kwa
    nini? Unasema umemuibia Mungu, lakini hakuna mtu anaweza kumuibia
    Mungu? Hii haiwezekani, kwa nini
    useme umemuibia Yeye? "Yeye akanijibu, "Mimi nitakuambia historia yangu ... Nilikuwa kiongozi wa Kikristo,
    kwa miaka 20 nilimjua Kristo, lakini katika kipindi cha miaka 20
    Nilisema: fedha zote kutoka katika
    mafungu ya kumi na sadaka zangu zilikuwa zinakwenda kuwanufaisha
    wachungaji, lakini hivi sasa najuta kwa
    sababu nimejua kwamba hazikuwa kwa ajili yao, zilikuwa ni kwa
    ajili ya Bwana, na ndio maana nasema
    nimemuibia Mungu ... Wakati huu kuna watu wengi sana duniani
    wanaomuibia Bwana kama mimi. Wakati
    utakaporudi duniani, waambie wale watu wote ambao hawataki kutoa
    zaka zao na sadaka, waimuibie Bwana,
    vinginevyo, wao nao wataishia Kuzimu, na hakuna mwizi atakayeingia
    katika Ufalme wa Mbinguni. Nilijua Neno
    takatifu, sasa ninajutia na kutambua kuwa nilimuibia Bwana
    (Malaki 3: 8).. Waambie watu wakati
    wanapomtolea Mungu, basi wamtolee Bwana kwa upendo wa kweli
    ". (2 Kor 9: 7) ". Mtu huyu aliendelea kusihi , "Bwana nisamehe", na Bwana akamjibu, Umechelewa sana, hakuna tena nafasi kwa ajili yako" Nilimuuliza mtu huyu, "Lakini kwa nini
    wewe ulimuibia Mungu, kwa nini? Wewe
    ulijua vizuri sana kuwa hatuwezi kumuibia Mungu zaka na
    sadaka." Yeye akajibu, "Ndiyo, mimi nilijua vizuri sana, lakini kamwe sikufuata, sikufuata kwa sababu
    nilikuwa mtu wa kiburi sana." Kamwe usimuibie Bwana, toa zaka na
    sadaka kwa Mungu kwa sababu kile
    tunachotoa kwa Bwana Duniani si kwa ajili ya watu. Tunapotoa kwa Mungu
    kwa moyo wetu wote, ni kwa ajili ya
    Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Biblia inasema kwamba Bwana
    anatujaribu, imeandikwa vyema katika Malaki 3:8-10 Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi
    mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema,
    Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu. Ninyi
    mmelaaniwa kwa laana; maana
    mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote. Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo
    chakula katika nyumba yangu,
    mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama
    sitawafungulia madirisha ya mbinguni,
    na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. Kama unataka Mungu abariki maisha yako na
    familia kwa ukuu sana, Basi usimuibie Mungu. Ni wakati wa
    kumbariki Mungu, ili abariki maisha yetu. Bwana akasema, "Nitakuonyesha kitu tofauti." Baada ya kuondoka mahali hapo, Bwana alinikumbusha kitu ambacho alinionyesha kabla ya uzoefu
    wangu wa pili, karibia Novemba. Wakati
    huo, nilionyeshwa Selo kule Page 4 4 kuzimu, na Neno maalum. Neno 'ARVIERD' alionyeshwa
    Angelica. Utafiti unaonyesha kuwa ni
    Kiitalia cha kale, au Kilatini. Katika utafiti tuligundua ukurasa wa 400 wa
    maandiko ya kale kuhusu neno hili,
    linalozungumzia Kuzimu halisi. Sikujua maana ya hilo neno, lakini
    nilielewa kwamba lilimaanisha kitu fulani
    kuhusu Dini . Yesu alinichukua na kunirudisha
    sehemu ile ile, ili kuona selo hizo tena. Tulipoingia,
    niliona maelfu ya watu. Kulikuwa na wanawake wawili
    wamevaa nguo nyeusi. Nilimuuliza Yesu "Ni nani
    hao?" Nilisikitika kuona mtawa, na katika
    mikono yake walikuwepo nyoka wakubwa, ambao
    walitengeneza kitu kama msalaba na Rozari. Nikasema, "ni nini hii, kwa nini wako
    hapa?" Mmoja wao alizungumza kwa
    sauti ya huzuni akisema, " Nilikuwa mtawa Duniani, lakini sasa niko
    mahali hapa." Niliona jinsi alivyoanza kuomba na nyoka alifinya mikono yake. Katika mikono yake
    kulikuwa na maelfu ya minyoo. Bwana
    akasema, "Angalia na sikiliza maneno haya." Alianza kulia, "Oh Bwana! Siwezi kuvumiliana na hili tena,
    nataka kutoka nje ya eneo hili, sitaki kuwa hapa, tafadhali Bwana
    Niaidie, nisaidie!" Kisha nikaona mwanamke mwingine, na
    sehemu ya maisha yao nilionyeshwa katika aina ya fulani ya
    televisheni/screen. Niliona watawa jinsi ambavyo huwa kihualisia, na
    maisha yao ya siri. Niliona jinsi watawa hawa walivyo na mahusiano ya kingono
    na mapadri, na jinsi ambavyo baadhi ya watawa hawa walikuwa pia
    wasagaji. Niliona mengi zaidi, na sasa walikuwa wakijutia na kutubu. Lakini
    kwa bahati mbaya, kulikuwa hakuna tena nafasi nyingine kwa wao kutubu;
    walikuwa wamechelewa mno. Wale watawa wakasema, "Nenda na ukawaambie wale wote Duniani, wasije mahali hapa, tafadhali nenda na
    uwaambie wasije hapa." Page 5 5 Wakati mwingine watawa/masista na
    mapadri husema kwamba watamuomba Mungu ili
    aziondoe roho zilizo Purgatory. Lakini mimi nawaambia kweli, Uniamini au usiniamini. Hakuna mahali
    panapojulikana kama Purgatory. Purgatory ilitungwa tu na wanadamu,
    ilitungwa na mapapa. Biblia inasema wazi wazi kwamba kuna
    Mbinguni na kuna Kuzimu halisi. Yesu alinichukua mpaka
    maeneo yote hayo mawili, lakini kamwe sikuwahi
    kupelekwa purgatory. Yeye kwa uwazi aliniambia, "Purgatory haipo, nenda na uwaambie watu wafanye maamuzi
    yao wakati bado wako Duniani, kwa sababu wakati wakiwa
    na uzima, kuna nafasi ya kutubu." Watu wengi wanasema, "hebu tuombe,
    ili ndugu zetu waondoke purgatory." acha hiyo! Kwa
    sababu kama wao walikufa bila Kristo kule Kuzimu KAMWE
    hawatoki. Ni bahati mbaya lakini ni kweli, kuwa wako
    Kuzimu. Lakini kama walikufa pamoja na Kristo
    katika mioyo yao, basi wako uweponi mwa Baba yetu wa
    Mbinguni. Moyo wangu uumaa kujua kwamba nafsi/roho
    nyingi sana zinadanganywa na shetani katika
    kuamini purgatory. Rafiki yangu ni wakati wa wewe kujua
    ukweli, purgatory haipo, yaani ni haipo. Inakupasa
    kufanya uamuzi sasa, ni wapi na na nani ambaye ungependa
    kuishi milele? Unaweza kufanya uamuzi wako mwenyewe, kama
    ni Ufalme wa Mbinguni na Yesu Kristo au Kuzimu na
    shetani. Bwana aliniagiza niseme moja kwa moja bila
    kupoza ninapowaambia hili, iwe unaamini au
    hauamini.Ninatii amri ya Bwana kwa sababu siku moja wewe na mimi tutasimama mbele ya Mungu, na kushuhudia yote mema na
    mabaya tuliyofanya hapa Duniani. Kama hautatubu dhambi yako
    na kuabudu kwako sanamu, utaishia kuzimu. Rejea kwa Kristo;
    Atakupa uzima wa milele. Sitaki kuwatisheni, lakini ni ukweli. Neno
    la Bwana li wazi sana na linasema kwamba hakuna mwizi
    atakayeingia mbinguni. Bwana alinionyeshea kwamba ndani ya kila
    picha / sanamu kuna pepo. Ndiyo maana watu huja kwa bikira wa
    Guadalupe(Virgin of Guadalupe ) , Bikira wa Sinema, Sanamu ya Bikira Maria na
    bikira wengine wengi 1 2 3 4. Hata sanamu ya 'Mtoto Yesu'. Tafadhali
    niamini mimi, hizi sanamu zote zina pepo nyuma yake. Watu wengi
    wanadai kuwa walikwenda kwa Bikira wa Guadalupe au Mtoto Yesu na
    kupokea uponyaji. Lakini miongoni mwa kila moja ya picha/
    sanamu hizi kuna pepo. Shetani
    anasikiliza na kwa nguvu zake za uongo, Page 6 6 wakati mwingine anafanya ionekane
    kama muujiza umetokea, ili uendelee
    kuamini na uendelee kumuabudu yeye. Nisikilizeni, shetani anaenda
    kukulipa wewe vibaya na atakupa mauti
    ya milele. Hivyo acha kuabudu picha umtafute Kristo, kwa sababu
    atakupa maisha ya milele na uzima kwa
    wingi (Yohana 10:10). Bwana alinionyesha watawa hao, nao
    walikuwa wakilia, "Nataka kutoka hapa, najutia kuabudu sanamu, na kufanya dhambi duniani, sasa siwezi
    kuondoka mahali hapa." Nilimuuliza mmoja wao, "Lakini wewe uliijua kweli? Ulijua Neno la Mungu takatifu?"
    Yeye alinijibu, "Ndiyo, nilijua Neno Takatifu, lakini kamwe sikutubu, kamwe sikumtafuta Kristo. Kuna watawa
    wengi walioamua kuwa hivyo kwa
    sababu nyingi. Mimi nilikuwa muongofu/hivi kwa sababu ya uchungu
    nilioupitia katika mauhusiano wa
    kimapenzi. Kuna watawa wengi kwa sababu ya kukatishwa tamaa katika
    mapenzi. Katika kesi nyingi, wachumba
    wao waliwaacha katika harusi madhabahuni, au marafiki zao wa kiume
    waliwasaliti, watawa wengi kwa bahati
    mbaya wapo katika kiapo kwa sababu maisha yao yamejaa
    matatizo na wito huu wanautumia kama
    sababu tu. Ukweli halisi ni kwamba wao wanamtumikia shetani. " Neno takatifu la Bwana linasema katika 1 wakorintho 6:9-10 " Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi
    ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi
    ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala
    watukanaji, wala wanyang'anyi.watakaorithi ufalme wa
    mbinguni. Neno lake takatifu liko wazi, Ufunuo 21:8 " Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji,
    na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo
    mauti ya pili. Page 7 7 Watu wote kule kuzimu hawana namna
    ya kutoka, kwao wamechelewa sana.
    Lakini Ninyi ambao mko hai katika dunia, bado mnaweza
    kupatanishwa na Mungu. Usikose nafasi
    hii, labda wewe hivi sasa unaangalia hii, na inaweza kuwa nafasi yako ya mwisho
    ambayo Mungu anakupa ili utubu. Epuka
    kuzimu, kwa sababu Kristo ananyoosha mkono wake wa rehema
    kwako. Tulipokuwa tunaondoka katika selo
    nilianza kulia kwa sauti na nilikuwa
    nikisema, "Bwana nitoe nje ya hapa, Bwana, mimi sitaki kuwa hapa." Alinitoa
    nje na kusema, "Nataka kuonyesha zaidi ..." Tulipokuwa tukitembea, nikasikia mayowe ya
    msichana mdogo, "Nisaidie! Nisaidie!" "Wewe ni nani? Kwa nini uko hapa?" Nilimuuliza. Msichana alijibu, "mimi ni kijana, nilikuwa nina miaka 15 tu wakati nilipokufa, na kuja mahali hapa." "Lakini kwa nini uko hapa? Nini kilichokuleta wewe
    hapa?" Nilimuuliza. Akasema, "Mimi nilifikiri nilikuwa na maisha mbele yangu, kwa sababu
    nilikuwa mdogo sana. Watu siku zote waliongea
    nami kuhusu Kristo na wokovu, lakini nilisema
    kwamba Wakristo wa hizo injili walikuwa vichaa/
    wehu, wakati wote nililikataa Neno Takatifu.
    Sikutaka kumkubali Bwana. Kila wakati
    walipozungumza na mimi, niliwacheka na kuwadhihaki.
    Sasa naona kwamba nilifanya makosa makubwa ya
    maisha yangu. Niangalie wakati huu
    niko mahali hapa ninaungua katika moto. Nilikufa katika ajali ya gari
    na sasa ninajutia sana. Nimekuwa
    nikitafuta njia ya ktoka hapa mara nyingi, na mara ninapoiona njia hiyo
    siwezi kutoka, kwani mapepo
    yanayonitesa yanasema, 'huwezi kuondoka mahali hapa, wewe ni hapa milele. 'Sitaki kuwa hapa, oh tafadhali
    nisaidie, nisaidie! "Mimi nikasema, "Siwezi kufanya kitu chochote
    kwa ajili yako, Ninatamani
    ningewasaidia watu wote hawa." Bwana akasema, "Hakuna nafasi kwa wale ambao wako hapa, lakini kwa
    wale tu walio Duniani." Msichana huyo akasema, "Oh tafadhali nenda kawaambie watu, na hata familia
    yangu wasije mahali hapa. Nenda kaseme na vijana ambao bado
    wana nafasi ya kumtafuta Kristo,
    waambie wageuke wawe mbali na dhambi. Nilipokuwa duniani, niliishi
    maisha ya ovyo, maisha yaliyojaa
    dhambi, nilikuwa na kiburi sana, nilifurahia kwenda kwenye pati/starehe
    za kila namna, kamwe sikuwatii wazazi
    wangu, nilikuwa muasi siku zote.Sasa ninajuta sana, na ninawataka
    wanisamehe. , ninataka kutoka hapa,
    mwambie kila mtu juu ya uso wa nchi asije hapa, asije, tafadhali.
    Waambie wawatii wazazi wao,
    wamkubali Kristo, kwa sababu kweli
    anaokoa, yeye kweli anaokoa, shetani
    alinidanganya, sasa najua siwezi milele
    kutoka mahali hapa,ni jinsi gani ninajutia. " Alilia na kunyoosha mikono yake,
    nilitaka kumsaidia lakini wakati ninampa
    mkono wangu aushike, yeye alianza kulia na tena katika moto. Nililia,
    "Bwana, ni namna gani inavyotisha
    kuwepo mahali hapa" Akanijibu, "Ndiyo Binti, kumbuka hili, nenda
    Duniani na utii amri yangu, ili
    wanadamu waamini kwamba Kuzimu
    ni halisi na ni milele, kwa sababu bado
    kuna wengi ambao hawaamini katika
    Kuzimu , kuna wengi ambao wanasanifu na kuleta mzaha
    wakisema kwamba kuzimu ni ya
    kufikirika. " Page 8 8 Siku chache kabla ya uzoefu wangu wa
    kwanza katika kuzimu Bwana alinipa maono na kusema, "Angalia, mtu huyu amekwenda kuzimu." Nazungumzia mtu maarufu anayejulikana kama MJ (Michael Jackson), yeye pia
    alijulikana sana kwa glove yake nyeupe. Alikuwa kuzimu kwa
    sababu ile niliyoieleza katika video yangu ya awali. Nilipokuwa
    nikirekodi video hiyo, Bwana aliniambia, "Sema kuhusu yeye." Ndiyo maana ninawaambia kuhusu yeye kuwa yuko katika miali ya
    Kuzimu. Wakati nakaribia sehemu hiyo ya moto,
    niliona pepo wengi wakiwa katika mduara, na ndani ya
    mduara huo kulikuwa na mtu aliyekuwa akiteswa. Alinyoosha mikono
    yake na kulia kwa sauti, "Msaada! Msaada!" Niliweza kuelewa lugha aliyokuwa akizungumza. Nilitaka kumsaidia sana, niliweza kuona
    jinsi mapepo yalivyokuwa yakimnyanyua na
    kumlazimisha acheze na kuimba kama
    alivyokuwa akifanya Duniani. Mapepo yalimdhihaki na kumtupa ndani ya moto.
    yalimchukua tena na kumchapa mijeledi.
    Alilia kwa maumivu ya kutisha. Oh, ni jinsi gani alivyokuwa
    akiteswa. Ilivunja moyo wangu kuona hili na
    nikasema, "Bwana, tafadhali fanya kitu,
    oh! Bwana msaidie." Niliponyoosha mkono wangu kumsaidia,
    mikono yangu ghafla ikawaka moto, na
    kujaa na minyoo. Nikasema, "Bwana Tazama! Nini kinatokea?" Kisha
    mapepo yalianza kucheka na
    kunidhihaki, "Wewe unakwenda kukaa mahali hapa." Kisha niligundua siwezi kuona au kuhisi
    kama Bwana yu karibu na mimi,
    ilionekana nilikuwa peke yangu. Nililia, "Bwana, umeondoka, kwa nini
    bado ningali hapa?" Mapepo yalisema, "Tunakwenda kukuadhibu, utakaa hapa." Kisha nikasikia sauti ya kuogopesha, ilikuwa ya kutisha, "Ha ha ha, wewe unakwenda kukaa hapa. Hatimaye nimekukamata, mahali
    muafaka ninapokuhitaji. Ninakutaka wewe hapa kwa sababu wewe umeiba roho nyingi kwangu na
    nitakuangamiza, hapa ndio kwako.
    "Alitoa amri kwa mapepo, "Mchukueni, na mpelekeni mahali panapomstahili." Nikajibu, "Hapana, hapana, mimi sitakaa
    hapa kwa sababu Bwana yu pamoja
    nami. Yeye alisema hawezi kuniacha hapa." Kisha nikasikia sauti ya
    Shetani "Wewe utakaa hapa, utakaa hapa kwa sababu Bwana hayuko na wewe. Angalia kote, hayuko
    na wewe." Nilitazama, lakini sikuweza kumwona Bwana. Nilijisikia Mpweke, na nilianza kuwa na mashaka.
    Nilianza kulia na kupiga kelele, "Bwana,
    kwa nini umeniacha? Kwa nini Bwana, kwa nini?" Mara Bwana akasema, "Binti, mimi niko hapa." Nilisikia sauti yake katika masikio yangu. Nilimuangalia moja kwa moja shetani, Nikamjibu,
    "Bwana yuko hapa pamoja nami." Lakini
    yeye alijibu, "Hakuna hayupo, wewe angalia." Sikuweza kumuona Yesu, lakini niliweza kusikia sauti yake.
    Nilianza kuwa na mashaka tena kwa sababu mapepo yalikuwa
    yananisogelea. Nilihisi kamba
    imefungwa kiunoni mwangu ambayo
    ilinivuta kuelekea kwenye ile sauti ya uovu.
    Ilisema, "Wewe ni mpumbavu, ndivyo ulivyo, mpumbavu sana. Nitakuharibu kwa sababu umesababisha
    roho nyingi sisije kuzimu, roho nyingi
    zinatoka nje ya kuzimu kwa Page 9 9 sababu wewe unahubiri. Usifanye hivyo
    tena, funga mdomo wako, yaani funga
    mdomo wako, nitakuangamiza, nitakuua. " Niliendelea kulia alipokuwa akinishitaki.
    Ghafla nikamjibu, "Hapana shetani,
    huwezi kuniharibu mimi, kwa sababu Bwana amesema yuko pamoja
    na mimi. Siwezi kumwona, lakini najua
    kwa hakika Yeye yuko hapa." Shetani anaendelea kunicheka. Nilikuwa navutwa kuelekea mahali
    fulani, karibu na ile sauti mbaya.
    Nikasema kwa sauti, "Damu ya Yesu ina nguvu na mimi nimefunikwa na damu
    yake, imeniunika hata sasa na shetani
    atakimbia mbali kwa sababu damu ya Yesu iko juu yangu. Mkubwa
    zaidi ni Yeye aliyepamoja nami zaidi
    yako. Mkubwa zaidi ni Yeye aliye pamoja nami. "Niliendelea kurudia
    maneno haya. Kisha niliona kitu
    kimeniachia; kama kitu kimenivuka, ilikuwa ni ile kamba iliyofungwa kiunoni
    mwangu. Hatimaye, nilitoka Kuzimu, na
    kurejeshwa katika uwepo wa Mungu.
    Bwana akasema, "Nataka nikupe ujumbe huu mara utakaporejea Duniani, nenda na uwaambie watu wangu
    wanitafute katika Roho na Kweli
    (Yohana 4:24). Nenda uwaambie watu wangu waishi
    katika utakatifu. Nenda na
    uwaambie watu wangu huu ni wakati, ni wakati
    wa kutafakari Neno Takatifu. Si tu nawataka watu wangu wasome,
    lakini pia wameze Neno langu
    Takatifu. kwa sababu Binti, hiki ndicho
    kinachotokea Duniani, Duniani kila
    siku uasi wa dini(apostasy)
    unaongezeka, bado kuna wengi wa
    watoto wangu, wengi wa watu wangu wateule
    wanadanganyika. Binti, waambie
    watu wangu wameze/kulishika neno langu
    Takatifu ili wasidanganyike na
    wautafute uwepo wangu katika roho na kweli. " Mimi nikasema, "Oh! Ndiyo Bwana.
    Nitatii. Lakini Bwana, nahitaji msaada
    wako, tafadhali nisaidie Bwana." Alijibu, "Binti, wakati utakaporejea, Usiwe na hofu kwa sababu
    nitasimama na wewe. Nitasema kupitia mdomo wako kile nimesema kwa
    watu wangu. Nimeona wengi
    wakiinuka kinyume dhidi yako, lakini kumbuka nitakuwa pamoja nawe
    daima kama nilivyoahidi, na mimi ni
    shahidi wako mwaminifu. " Kisha nikaona malaika karibu yangu.
    Nilimtambua Malaika Mikaeli, kwa
    sababu nilikutana naye kabla. Bwana akasema, "Sikiliza, malaika Mikaeli atakwenda kukuonyesha
    kitu". Malaika Gabrieli pia alikuwa pembeni mwangu. Kisha malaika Mikaeli
    akachukua mkono wangu, na Bwana
    akamwagiza, "Mchukue na umuonyeshe kile imekupasa
    kumuonyesha." Tulipokuwa tunatembea, tulianza
    kupanda juu ya ngazi nzuri sana.
    Ilionekana kama chumba cha mpira. Na katika sehemu ya juu ya chumba
    kulikuwa na madhabahu ilyokuwa na
    mimbari nzuri sana ya dhahabu. Tulipofika katika mimbari, nikaona
    kitabu kikubwa na nikamuuliza Mikaeli,
    "kitabu hiki, ni nini?" Wakati Mikaeli alipokuwa upande wa
    kulia wa mimbari, aliweka mkono wake
    juu ya kitabu na kusema kwa sauti yake, "Angelica, kitabu hiki unachokiona hapa ni Kitabu cha
    Uzima". Nilikifungua na nikaangalia ukurasa kwa ukurasa .Nikasema, "Je,
    kitabu hiki kina maana gani, Ni mambo
    gani yaliyoandikwa ndani yake?" Mikaeli akasema, "Fungua, ndani ya kitabu hiki yameandikwa
    majina yote ya wale ambao Duniani wametubu na wakageuza maisha
    yao kumuelekea Baba yetu wa
    Mbinguni." Page 10 10 Nilipokuwa nikiangalia ndani ya kitabu,
    Nilimuuliza Mikaeli, "Je, jina langu limeandikwa hapa?" "Ndiyo, angalia hapo juu na utaliona." Niliangalia, lakini sikuweza kuliona. Nikawa na wasiwasi kidogo, Nikauliza, "jina langu
    haliko hapa, silioni, liko wapi?" Yeye alinijibu, "Angalia, jina lako ni hili." Nilifurahi kuona jina langu, lakini
    sikuweza kulielewa ni kwa sababu lilikuwa limeandikwa katika
    lugha nyingine. Niligundua kuwa majina mengi yalikuwa
    yanang `aa, hivyo nikamuuliza," Kwa nini majina yale
    yanang'aa na Kuwaka? "Yeye alijibu, "Majina haya unayoweza kuona yaking` aa katika
    kitabu cha uzima, ni watu wale
    waliopo Duniani, kwa wakati huu hivi sasa
    wanatubu dhambi zao na kutafuta
    uwepo wa Mungu. Tazama, majina haya mengine ambayo ni vigumu
    kuonekana na baadhi yao yanafutwa
    kama ilivyo tayari kwa wengine wengi, ni watu wale duniani ambao
    wamegeuka mbali na njia za Mungu.
    Inakupasa ufanye jambo, fanya jambo! " Kwa mara nyingine tena, akaweka
    mkono wake juu ya kitabu cha uzima na
    kuniambia, "Enenda ukawambie wanadamu kuwa kama majina yao
    hayakuandikwa katika kitabu hiki,
    hawawezi kuingia katika Ufalme wa Baba yangu wa Mbinguni, hawawezi
    kuingia katika Ufalme wa Mbinguni .
    "Mimi nikajibu, "Sawa, nami nitafanya hivyo." Imeandikwa katika
    Ufunuo 20:15 "kama jina la mtu yeyote halikuonekana katika kitabu cha uzima, alitupwa katika ziwa la moto." Tulitoka nje na kurudi kwa Yesu,
    alisema, "Ni wakati wa wewe kurudi Duniani." Je, unafikiri jina lako limeandikwa katika
    kitabu cha uzima? Kama hudhanii hivyo,
    nenda na umtafute Mungu. Kama umemgeuka Mungu,
    patana naye, kwa sababu yeye yuko
    tayari kukusamehe, bila kujali umefanya nini. Kumbuka, alikuja kuokoa
    wenye dhambi; Yeye alikuja kusamehe
    dhambi za wanadamu wote duniani. Wewe fungua moyo wako na
    umsihi akusamehe. Yeye yuko tayari
    kutusafisha na udhalimu wote, kama inavyosemwa katika 1 Yohana 1: 9 'Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni
    mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha
    na udhalimu wote'" Nilipokua nikirudi Duniani, niliona mwili
    wangu umelala pale. Ilikuwa ni asubuhi na mapema, karibu
    saa 01:00 asubuhi. Katika nyumba yangu, niliweza kuona familia
    yangu na baadhi ya washirika wa kanisa. Bwana akasema,
    "Binti, ingia kwenye mwili wako, ingia kwenye mwili wako,
    fanya hivyo sasa", "Sawa Bwana," nilijibu. "Kumbuka hili, utakuwa na mafunuo
    mengi yanayotoka kwangu, na hivi karibuni utakuwa na
    ufunuo wa tatu kuhusu nini kinatokea ndani ya watu wangu.
    Kumbuka tu mimi nipo pamoja nawe." Ghafla niliona mwanga na Malaika walianza kuimba. Baada ya masaa mengi,
    hatimaye niliweza kufungua macho yangu. Ilinichukua muda wa siku
    nyingi kupona kabisa. Mimi nataka ujue kwamba kila kitu
    ulichosikia kwenye video hii sio hadithi
    ya kufikirika, Bwana aliniruhusu nipate uzoefu huu. Nataka ujue kama
    unahitaji Mungu akusamehe, basi fumba
    macho yako na weka mkono wako wa kulia juu ya moyo wako na
    uombe, sema kwake, Page 11 11 "Bwana Yesu, Ninatubu dhambi zangu
    zote, Ninatubu kwa sababu mimi
    nimefanya dhambi kinyume chako, Nakusihi wewe Bwana unisamehe
    dhambi zangu na unisafishe kwa damu yako ya thamani, Nakusihi
    uandike jina langu katika kitabu cha uzima. Nipige muhuri kwa Roho
    wako Mtakatifu wako, Ingia na ukae katika maisha yangu na
    unitakase na uovu wote. Nakataa tamaa za mwili wangu. Nakana maisha
    yangu ya zamani, na yote yale ambayo hayakupendezi wewe,
    Natangaza leo, kwamba minyororo yote iliyonifunga kwamba
    ifunguke, Niko huru, kwa sababu umeniweka Huru. Kwa jina la
    Yesu, Amen "" Amani ya Mungu iwe ndani ya mioyo
    yetu, na ukumbuke kwamba ni Roho Mtakatifu, na Roho Mtakatifu
    pekee ndiye ambaye anatushudia hatia ya dhambi zetu.
    Mungu awabariki. Angelica Zambrano Mora ---------------------------------------------- Kama unataka kuwa sehemu ya huduma
    hii unaweza wasiliana nasi kwa barua
    pepe zifuatazo : esdios@hotmail.com palabraderevelaciondivina@hotmail.com (Kama inawezekana, tumia Kihispania) ** Toleo hili ni Minimally Abridged,
    Polished na Illustrated. Video ya awali katika lugha ya
    Kihispania . Ndugu aliyefasiri ufunuo wa 2 kuhusu
    mbinguni na kuzimu wa Angelica
    Zambarano ni Peter Kahale ni kijana aliyeokoka na anampenda Yesu na
    mwenye shauku ya kuhubiri injili ya
    Yesu Kristo. Simu ya Mkononi: +255-755-255043,
    +255-653-610460. Barua Pepe: kahalepeter@gmail.com

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate