Wafilipi 2:10-11
  • JINSI SADAKA ZA WANA WA MUNGU ZINAVYOIBIWA WAKIFIKIRI WANAMTOLEA MUNGU NA KUMBE WAMEIBIWA PESA ZAO NA



    JINSI SADAKA ZA WANA WA MUNGU ZINAVYOIBIWA WAKIFIKIRI WANAMTOLEA MUNGU NA KUMBE WAMEIBIWA PESA ZAO NA WATUMISHI.

    BWANA YESU ASIFIWE. YESU WA NAZARETI aliye hai, tena anawapenda watu wote wabarikiwe kupitia njia ya sadaka na siyo watu waibiwe sadaka zao wakifikiri watabarikiwa kumbe wameibiwa na baadhi ya watumishi ambao ni wanadamu kama wewe tena pasipokujua wewe muumini ila mtumishi anakuwa anajua kabisa yeye ni mwizi wa pesa za watu na anatumia jina la YESU kupatia pesa.

    Katika kazi ya YESU aliponiita pale mwanzoni ilikuwa vigumu mimi Hebron kumwelewa ila siku zilipoongezeka kwa neema yake niliweza kumwelewa YESU vizuri kwa sababu katika mambo mengi niliyoyafanya katika kumwabudu yeye kama mtu mkristo asilimia kubwa sana akaniambia sivyo, yapo kinyume  na yeye, akanifundisha kisha akanituma sasa kwa mataifa yote niwaletee watu habari njema za wokovu na kuziondoa habari mbaya za wokovu walizozipokea au habari mbaya za ukristo walizozipokea ikiwa wanamaanisha mafundisho ya uongo ambayo watu wamefundishwa kwa njia ya mapokeo na wengine hata watumishi hawajui na kuwafanya na wao wapotee na cha ajabu ukisema ukweli baadhi hawataki kwa sababu wamenogewa na ukristo potofu ila wachache hufurahi na kutubu kwa sababu   wamepona roho zao na wanaona kabisa biblia hajaruhusu mambo hayo.

    Katika kipengele hiki ninaelezea zaidi katika swala la sadaka ambazo anaibiwa MUNGU pamoja na muumini na kufanya asifanikiwe katika maisha yake japo muumini yeye anampenda YESU ila anakutana na geiti la kuibiwa sadaka zake na matokeo yake maisha yake yanakauka haoni neema ya MUNGU katika kila jambo kupitia sadaka zake. Sadaka hizo zipo namna hii:

    a.      Sadaka kuandika jina, kiasi chochote, email address yako na kisha unapewa risiti kanisani. Hapo tayari umeibiwa pesa yako na siyo sadaka iliyopokelewa na MUNGU. Sababu ya kwanza sadaka ni siri yako na MUNGU peke yake, sasa tazama siyo siri tena na MUNGU, hivyo shetani anamnyanyuliwa MUNGU mashtaka tazama siyo siri tena inajulikana na wanadamu na neno lako halijaruhusu itolewe kwa jinsi hiyo.

    b.     Sadaka unazoambiwa utoe kiasi fulani halafu ndiyo uombewe na ndipo utafanikiwa hiyo tayari unaibiwa pesa yako kabisa, wala haitazaa baraka zozote kutoka kwa MUNGU.

    c.      Sadaka za mavuno; hii ni sadaka ya fungu la kumi la mazao uliyoyapata hivyo haina tofauti na mshahara wako unaoupata baada ya kulipwa mshahara wako. Kile kitendo cha kufanywa mnada mazao ya mtu kanisani ili iongezeke, ile ni njia ya shetani ya kumvurugia mtu fungu lake la sadaka ya kumi liharibike na zaidi unakuwa ni mwizi wa fungu la kumi hata kuhani anayeshiriki hayo MUNGU anamwita yeye ni mwizi wa pesa za watu na zaidi mbinguni anaitwa yeye na kanisa hilo ni mahali pa wanyang’anyi na pia katika ulimwengu wa roho iyo dhambi inawafuatia kwa sababu hiyo ni roho ya shetani na inakaa mahali ambapo inapewa nafasi ya minada ya mazao.

    d.     Sadaka za kukanyagwa miguuni na mtumishi anaziombea hiyo inayomaana kuwa anakanyaga baraka zako, mafanikio yako na wokovu wako na hautasimama kiroho na zaidi watumishi wanaofanya hayo ni maagano ya masharti waliyopewa na shetani katika kitengo cha roho ya mpinga  kristo ili kuharibu maisha na roho za watu ziangamie kwa kupitia mpinga kristo na watu hawajui.

    e.      Sadaka ambazo watu wanatumiwa kwa meseji ya simu au email zinasambazwa kwa njia ya mtandao, mfano mtumishi anasema hivi, naona utalia au kupita tatizo kubwa sana hivyo tuma kiasi hiki cha pesa ili niombe hilo tatizo liondoke. Nawaeleza hao ni waizi wa pesa za watu, mambo haya yametawala katika nchi mbali mbali wakitumia jina la YESU. Nawaeleza YESU amenieleza msitoe hao wanalitumia jina lake kunyang’anya watu vitu vyao na yeye YESU hata hawajui wala hana ushirika nao wowote ila wapo katika upande wa mpinga kristo na ndiyo sababu wanavyoendeleza na shetani.

    f.       Sadaka ambazo unakuta mtumishi anayasoma majina ya watu waliotoa sadaka tena madhabahuni na pia mtumishi anapotaka kujua unamtolea MUNGU kiasi gani. Yeye siyo MUNGU, hapaswi kujua kiasi unachotoa, ukikuta hali hiyo hata kama unaendelea kutoa miaka yote unaibiwa pesa zako na usitegemee baraka za MUNGU. Jichunguze maisha yako na uangalie uaminifu wako kwa MUNGU halafu why mambo hayaendi? Umeibiwa na mwanadamu.

    g.      Kudaiwa malimbukizo ya sadaka ulizoshindwa kuzilipa mfano walipojua unapata kiasi gani kwa mwezi hivyo unawekewa file lako la rekodi yako na kila mwezi wanapiga tick kama umelipa na kama haujatoa unaadikiwa haujatoa hivyo pesa yako inakuwa deni na utadaiwa na zaidi utaambiwa unadaiwa na MUNGU umemwibia embu angalia hii hekima ya shetani wanavyoitumia na watu wanaamini, rudi katika mifano ya biblia hakuna kukaguana unalipa kiasi gani, ukimwibia MUNGU hiyo ni wewe na MUNGU utajuana na yeye. Sasa shetani anatumia njia hii kuwateka watu fikra zao na kuwafanya makampuni au hisa zao pasipo wao kujua na wengine wameshashuhudiwa na ROHO MTAKATIFU kabisa hiyo siyo sawa ila hajapata uhakika mimi nakuhakikishia usishiriki hayo tena utapona roho yako na uchumi wako.

    h.     Sadaka za kutoa kwa miungu harambee michango makanisani katika nyumba ya sala sadaka hizo hata kama unaona unamfanyia MUNGU tayari ni machukizo kwa MUNGU, nyumba imeshkuwa ni soko ukataka kumtolea MUNGU wewe fanya siyo utengenezewe mazingira. Hizi sadaka za kutengenezewa mazingira zote ni za kuwaibia wana wa MUNGU pasipo wewe kujua na pasipo wewe kujua na hazipokelewi kwa MUNGU hata zikiombewa kwa jina la YESU, tazama sadaka ya Kaini na Abel wote walitoa kwa MUNGU angalia sadaka ya Abel ndiyo iliyopokelewa na ya Kaini haikupokelewa na hata sasa kina Abel wa leo ni wachache sana ila wengi zaidi sadaka zao zinakuwa kama za Kaini hawaoni baraka. Sasa uelewe wewe unayotoa hauna shida, shida ipo kwa kuhani uliyotolea sadaka zako na madhabahu ndiyo sababu hausongi mbele unazidi kuporomoka kiroho na kimwili, na kumbe sadaka yako haineni kwa MUNGU bali ipo upande wa adui na wewe haujui.

    i.        Kila sadaka unayoambiwa utoe ili uombewe ndiyo MUNGU atakuponya huo ni uwizi na pia unaambiwa utoe ndiyo utamwona mtumishi kwa private huo ni uwizi, hizi zote unaibiwa na hata ukitoa hubarikiwi na MUNGU na pia yeye hahusiki katika maongezi hayo bali sababu yeye neno lake nimekupa bure toa bure. Na sadaka nyingine pia ya kuchajiwa kiwango fulani utoe halafu umwagiwe mafuta ya baraka pia hiyo ni njia ya kuibia watu pesa wakifikiri wanatoa sadaka ili wabarikiwe. Hiyo ni kazi ya uwizi ya kuwaibia watu pesa zao kupiti jina la YESU. YESU anarudi kulinyakua kanisa muda wowote ndivyo alivyoniambia na akasema walifikiri sitarudi, narudi, na hao wote wanaoendelea hivyo mahali pao ni shimo la moto wa jehanamu kwa sababu wanalifanya jina lake litukanwe na YESU aonekane ni mnyang’anyi, mwizi na yeye hayupo hivyo. Na zaidi aliniambia hajatuma watumishi kunyang’anya watu pesa na mali zao bali kueneza injili ya kweli basi. Ila sasa imebadilika asilimia kubwa injili yake imeharibiwa, watu wamefundishwa injili ya uongo na wameipokea, na pale tu wanapoipokea mimi siko nao wanakuwa na shetani. Tubuni na mrejee.

     Sasa upone katika jina la YESU WA NAZARETI sema BWANA YESU naomba rehema, nimeujua ukweli sitakubali tena kuibiwa pesa zangu tena. Uniongoze wewe pa kukutolea ili unibariki na unifundishe kupitia ROHO MTAKATIFU, uandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele, na utakapokuja usiniache YESU.

    Zaidi soma vitabu vya Nabii Hebron utaelewa zaidi na utakuwa huru.

    NABII HEBRON.

    Hakuna maoni:

    Visits

    Translate